Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, upatikanaji wa dawa za kuua wadudu ni changamoto hasa vijijini, dawa hizi pia zitolewe kama ruzuku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upatikanaji wa pembejeo za kilimo kama mbolea katika Wilaya hasa Wilaya ya Kyerwa bado ni changamoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, power tiller zitolewe wa mkopo katika vikundi na walipe kidogo kidogo kwa wakati tofauti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uimarishaji wa masoko ya mazao ya wakulima hasa yale yanayooza kama nyanya, matunda na kadhalika. Wananchi wamezidi kupata hasara kwa kuwa haya mazao yanakuwa hayatunzwi muda mrefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuendeleza zao la maua (hot culture). Hii ndiyo namna kuu tutakayoweza kupata pesa ya kigeni na soko lake liko tayari hasa nchi za Ulaya kama wafanyavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo kubwa la mnyauko katika zao la mgomba (Wilaya ya Kyerwa). Ni kiwango gani Wizara imejipanga kusaidia wakulima hawa kutokomeza tatizo. Sambamba na hilo wananchi wanaokutwa na migomba iliyo nyauka wamekuwa wanatozwa fine. Hii ni sawa na kuweka chumvi kwenye kidonda.