Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, wakulima wa tumbaku wanapitia kipindi kigumu sana kuhusu masoko na bei ya zao hili. Najua kuwa Serikali inafanya kila njia kuwasaidia wakulima katika hili. Pamoja na hayo wawakilishi wa wakulima wa tumbaku Kusini mwa Ikweta walikaa Lilongwe nchini Malawi na kutoa azimio la pamoja lenye maslahi ya kuwalinda wakulima. Serikali italeta azimio hilo Bungeni lini ili Bunge liweze kuridhia?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba sana Serikali ifanye haraka kuleta azimio hilo Bungeni. Naunga mkono hoja.