Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Joshua Samwel Nassari

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. JOSHUA S. NASSARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza kwa yale mliyofanikiwa ndani ya Wizara lakini pia nawapa pole kwa yale ambayo yamekwama kwa namna moja ama nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, one thing, wananchi kwenye maeneo ya milimani waliokuwa wanalima zao haramu la bangi kama zao la biashara na hivi ndivyo ambavyo wameweza kusomesha watoto na kujikimu kimaisha. Serikali kupitia Bodi ya Pareto waliahidi kuanzisha zao hili kama zao mbadala na iliahidiwa kuwa elimu ingetolewa na miche ingetolewa mapema mara tu mvua za masika zitakapoanza. Mvua zilianza mwanzoni na katikati ya mwezi Machi lakini mpaka mwezi wa nne bado hakukuwa na lolote. Tafadhali naomba kauli ya Wizara katika hili ukizingatia kilimo cha bangi kilikuwa kwa sababu za kibiashara hususan kwenye nchi jirani na walikuwa wakitegemea kilimo hiki kwa
livelihood yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, otherwise, all the best.