Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na tatizo la mbolea kwa Wilaya ya Ludewa. Mbolea ya kupandia inachelewa kufika kwa wakulima na matokeo yake uzalishaji wake unakuwa hafifu na pia mbolea hiyo inauzwa kwa bei kubwa mno tofauti na bei elekezi iliyotolewa na Serikali. Serikali ije na mfumo madhubuti wa upelekaji kwa wakulima mbolea inayohitajika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu masoko ya mazao, wakulima wa Tanzania wanazalisha mazao kwa wingi mno na hasa pale Serikali inapotoa hamasa kwa wakulima kufanya hivyo. Serikali ichukue hatua ya utafutaji masoko kwa wakulima wetu hasa masoko ya nje mazao kama mahindi, maharage, viazi na kadhalika. Wakulima wetu wasaidie kutafuta masoko kwani kutofanya hivyo kuna shusha morari kwa wakulima wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ukulima kwa kanda (zone) Tanzania ina maeneo mengi ya ukulima wa mazao mbalimbali katika maeneo mbalimbali nchini, sasa tuanze mkakati wa kulima mazao kutokana na hali ya hewa husika katika maeneo husika. Mfano kuwepo na Kanda ya Nyanda za Juu Kusini kama center ya uzalishaji wa mazao ya chakula na kuwepo na mpango mahsusi ambao utaleta kilimo cha tija. Pia yawepo maeneo mahsusi ya kilimo cha miwa kwa ajili ya kuondoa tatizo la sukari, pia maeneo mengine (kanda) kwa ajili ya alizeti, karanga, mawese ili kuondoa tatizo la mafuta ya kula.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kila eneo likipewa zao maalum na jitihada ziwekwe ili kila kanda ifanye jitihada za ukuzaji wa mazao mbalimbali. Kilimo cha namna hii kikipewa kipaumbele tutajinasua na upungufu wa chakula na pia kutoa malighafi kwa ajili ya viwanda vyetu ili kuongeza thamani mazao ya wakulima. Kilimo kiki-link na viwanda vyetu, lengo la Serikali ya viwanda litafanikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uzalishaji wa mbegu, Serikali iweke nguvu za kutosha katika utengenezaji wa mbegu za mazao. Mbegu imekuwa changamoto kubwa, ifike mahali ziwepo center’s za utengenezaji mbolea hasa za kitafiti kutokana na ardhi mbegu hizo zinaenda kufanyiwa kazi.