Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa fursa hii. Nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa hotuba nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zao la nazi linapotea kwa kasi kubwa na nimepitia hotuba ya Mheshimiwa Waziri sijaona mikakati yoyote ya kufufua zao hili ambalo ni muhimu sana maeneo ya mwambao wa Pwani hususan Kisiwa cha Mafia, mkoani Pwani. Ninamuomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja kujibu hoja anieleze mipango kupitia utafiti ili kunusuru zao hili la nazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo cha utafiti wa kilimo kilichopo Mikocheni kina hali mbaya sana kifedha na Wizara bado haipeleki fedha ambazo kwa kiasi kikubwa itaokoa zao la nazi ambalo linazidi kupotea kutokana na minazi ya zamani kuanza kuzeeka na hakuna mipango mbadala ya kupanda miche ya kisasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo cha mwani kinacholimwa zaidi Kisiwani Mafia hakijapewa kipaumbele chochote katika bajeti hii. Miongoni mwa changamoto za kilimo hiki ni soko, mpaka sasa wananchi wa Mafia wamezalisha mwani mwingi na umerundikana katika maghala, changamoto nyingine ni vifaa duni wanavyotumia wananchi. Nimuombe Mheshimiwa Waziri awape zana za kisasa wananchi wa Mafia, hususani Kisiwa cha Jibondo ambao uchumi wao umeporomoka sana kutokana na katazo la kuvua wanategemea kilimo hiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna changamoto ya taaluma ya kisasa, tunaomba Serikali itupatie wataalam wa kuendesha mafunzo ya ukulima wa kisasa wa mwani. Ninashukuru na ninaunga mono hoja.