Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii ni pana inayohusika na idadi kubwa ya wananchi wanaoshiriki kwa upatikanaji wa chakula na kibiashara katika uchumi wa wananchi hao. Kutokana na uzito wa Wizara hii, sina budi kutoa shukrani za dhati na pongezi kwao Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watumishi wote wa kada mbalimbali kwa kazi nzito waifanyayo kuhudumia wananchi, pamoja na uchache wa bajeti yao na bado Wizara ya Fedha inawasilisha kwa fedha za miradi ya maendeleo kwa asilimia 18 kwa fedha zilizoidhinishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni hatari kwa watekelezaji na wasimamizi wa kilimo chetu nchini. Hivyo, Fungu 43 kwa mwaka 2017/2018 ya tengeo la shilingi 150,253,000,000 na kupelekewa shilingi 27,231,305,232.69 ambayo ni 18%. Tunaomba kwa mwaka 2018/2019 fungu hili liweze kutekelezewa kwa angalau 65% kama sio 75% kutokana na shilingi 162,224,814,000 ili tuweze kuboresha zaidi maendeleo ya kilimo chetu nchini na kuweza kuongeza pato la Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuendelea kusubiri mvua za msimu ambazo zinaendelea kupungua na kutokukidhi haja ya kuivisha baadhi ya mazao kwenye baadhi ya maeneo hapa nchini na kurudiarudia kila mwaka na wananchi wa maeneo hayo kupata shida ya upatikanaji wa chakula, kwani kinakuwa kwa gharama kubwa na wengine kushindwa kukipata na kuwasababishia kubadili utaratibu wa kutumia chakula kwa mlo mmoja kwa siku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara inafahamu maeneo hayo, lakini urasimu wa utekelezaji kwa wataalam wetu wa kuchukua muda mrefu wa utafiti wa kufanyia kazi kwa wakati bado maeneo hayo hayana mavuno mazuri. Wataalam waweke mikakati ya makusudi ya kukabiliana na uharibifu wa hali ya hewa kwa kujikita zaidi kwenye kilimo cha umwagiliaji kwa kuhakikisha maji ya mvua yanavunwa, tusikubali maji haya yakapotea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano Bonde la Rukwa linapokea maji mengi kutoka Ufipa ya Juu na kwenda moja kwa moja Ziwa Rukwa na kujaza udongo na kusababisha ziwa kujaa udongo na kina chake kupungua na maji kupotea. Maji hayo yakingwe kwenye mabwawa kadhaa yatasaidia kilimo cha umwagiliaji, maji ya kutumiwa na wananchi, mifugo na viwanda vidogovidogo na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala zima la ushirika kwa sasa wananchi wengi na ambao wanaumia na utekelezaji wa viongozi waliotangulia kutokutenda haki, hasa kipindi cha hapa kati, kunawakatisha tamaa kwa kuendelea na suala la kuendelea na ushirika. Ushauri ni bora sasa ukafanyika kwa kina uchambuzi wa viongozi wetu ndani ya ushirika kwa kila eneo hapa nchini, ikibidi tupate viongozi tofauti kabisa. Ushirika tulionao tuone utaratibu wa kuunda muundo tofauti na tulionao ambao hauna usimamizi na ukaguzi wa karibu na chombo husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kushukuru kwa jitihada zote zinazoendelea kwa kuendeleza kilimo, lakini bado uchelewesho wa mbolea na pembejeo kwenye maeneo kwa kuzingatia na msimu wao kuanza. Nashauri pembejeo na mbolea uwepo utaratibu wa kuwa ni bidhaa zinazokuwepo ndani ya maduka yetu mwaka mzima. Kwa kuwa ni mwanzo, tunaomba Wizara kutoa maombi Serikalini ya kusogeza huduma hiyo angalau kwenye kuunda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.