Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Zainabu Nuhu Mwamwindi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote naomba nianze kwa kumshukuru Mungu aliyeniwezesha kutoa mchango wangu katika Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Waziri wa Kilimo, Naibu Waziri pamoja na watendaji wote katika Wizara hii kwa kutekeleza vema majukumu yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe kuishauri Serikali kwa jicho la huruma imtazame mkulima wa zao la mahindi. Mkulima huyu ameteseka sana, amelima kwa taabu lakini anapofika kuuza mahindi yake anapatiwa masharti na kuzuiwa kujitafutia masoko likiwemo la kufanya mipaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie katika mambo mawili yanayohusu Wizara hii ya Kilimo kuhusu zao la pareto. Inafahamaika kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi tatu duniani zinazozalisha asilimia 90 ya zao la pareto. Kilimo cha zao hili katika Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania kimeweza kuwa mkombozi kwa wananchi kiuchumi na kukuza pato la Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niiombe Wizara isimamie kwa ukaribu ustawi wa zao hili katika Mikoa inayolima na hasa kufanya tafiti mpya zitakazobainisha maeneo mapya ya uzalishaji na kuongeza uzalishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, ahsante.