Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Risala Said Kabongo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. RISALA S. KABONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia hoja hii ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda haviwezi kuwa endelevu kama hakutakuwa na malighafi ambazo kimsingi zinatokana na kilimo. Waziri atakubaliana na mimi kwamba bila kuwa na mapinduzi ya kilimo ndoto ya Tanzania ya viwanda haitafanikiwa. Nasema hivi kwa sababu kilimo chetu bado ni duni sana kuweza kuzalisha malighafi za kulisha viwanda hivyo vinavyokusudiwa kujengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu zao la mbaazi, zao hili uzalishaji wake umeongezeka sana ambapo wakulima walizalisha tani milioni 2.3 za mbaazi mwaka 2016. Naiomba Serikali iendelee kuangalia kwa jicho la ukaribu soko la mbaazi ili wakulima hawa wasiendelee kupata hasara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mafuta, ninaamini kuwa wananchi wengi wanaelewa kuhusu utumiaji wa mafuta ya mbegu. Ninashauri Serikali itoe mikopo kwa wakulima ili waweze kuzalisha kilimo cha mbegu za mafuta na mafuta yatosheleze nchi nzima, sambamba na upatikanaji wa mashine kwa bei nafuu za kukamulia mafuta ili wakulima waweze kuuza mafuta na kupata faida kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri pia Serikali iendelee ku-support zao la apples katika Mkoa wa Njombe. Mwaka jana nilizungumzia suala hili naomba nilisemee tena kwa kuwa tumekuwa tunatumia sana apples kutoka Afrika ya Kusini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya kilimo iangaliwe kwa jicho la karibu ili kusaidia wakulima wetu hasa kuwafikia kutoa elimu ya mbegu bora na kilimo chenye tija.