Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Janeth Maurice Massaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. JANETH M. MASABURI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwapongeza Waziri wa Kilimo, Naibu Waziri wa Kilimo, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na watendaji wote walioshiriki katika kutenda na kusimamia shughuli zote zinazohusika na kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na pongezi hizo, kuna changamoto ambazo zinatakiwa kupatiwa ufumbuzi wa haraka ili kukidhi mahitaji ya Watanzania kwa kuzalisha mazao ya chakula na biashara kwa kupunguza uagizaji wa mafuta ya kula na sukari kutoka nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, iwapo nchi yetu itazalisha mazao ya mbegu za mafuta ya kula na sukari kwa kiwango kikubwa, kwa Serikali kuwekeza kwenye kilimo cha miwa na mbegu za mafuta kuongeza mashamba na kushiriki. Jeshi la Magereza, Jeshi la Kujenga Taifa na wawekezaji kutoka nje ya nchi na Watanzania wenyewe kwa kuweka mazingira mazuri ya kilimo, kuweka miundombinu ya umwagiliaji kama kuvuna maji ya mvua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kushirikisha nguvu kazi ya vyombo vya ulinzi itasaidia vijana wetu kushiriki kikamilifu katika kuzalisha mazao mbalimbali na pia itasaidia vijana kupata ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mazao makuu ambayo ni ya kiuchumi hapa nchini yanapaswa kuwekewa mkakati wa kudumu na endelevu kwa kuweka misingi imara. Kilimo cha kisasa cha umwagiliaji hakikwepeki katika zama za sasa.

Kilimo kiendane na dhana ya Tanzania ya viwanda kwa vitendo, kila Wizara inahusika na kushabihiana na Tanzania ya viwanda.