Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kunipa nafasi. Kulingana na muda niende moja kwa moja kwenye hoja. Nitazungumzia hoja chache. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo cha mahindi, Mkoa wa Rukwa unalima mazao mengi na hali ya hewa inakubali kuzalisha mazao mengi lakini mahindi yanalimwa kwa asilimia 43 ya mazao yote yanayolimwa pale na ardhi yote. Ndio kusema kwamba kilimo cha mahindi kwa Mkoa wa Rukwa ndiyo maendeleo yao kwa kila kitu kielimu, afya, watoto kwenda shule na kila kitu, lakini sasa tunaanza kukwama kutokana na kilimo kutokwenda vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kilimo hiki kinakwama kwenda vizuri kwa sababu ya mipango mimi niseme mibovu ya kuendeleza kilimo, haiwekwi vizuri. Sasa tunaanza kuona mwaka hadi mwaka hali inakuwa inabadilika, lazima tusimame tupaze sauti. Wakulima sasa wanangamizwa na ndiyo hao wanakaa kijijini ndiyo wanatuchagua na kutuweka kwenye madaraka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali ibadilike, mtazamo wa kilimo sasa si sawa hata kidogo. Kuna mawakala wamehudumia kilimo, si sawa kufikiria kwamba wote walikuwa wezi na kwamba kazi waliyoifanya haina maana, siyo sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie muda mfupi huu kuwasilisha kilio cha wakulima wa Vijiji vya Kasu, Kisula, Milundikwa na Malongwe. Wakulima hawa hawana shughuli nyingine ya kufanya kutokana na uamuzi wa Serikali wa kutwaa maeneo ya jeshi, wamekosa ardhi kabisa. Nitatumia muda mwingi kulisemea hili na leo nashukuru nimefanikiwa kumuona Waziri Mkuu nikamfikishia, najua limefika Serikalini, Serikali najua inasikia. Kwa huruma ya Serikali naomba jambo hili lizingatiwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo ni muhimu sana, leteni mbolea; Minjingu sisi hatuitaki, Minjingu haitakiwi, anayesema Minjingu fanyeni utafiti. Basi kama mnaitaka iwekeeni subsidy, muilete kwenye soko halafu wananchi waende kwa kupenda au kwa ubora wake na si kwa kulazimisha. Minjingu katika Mkoa wa Rukwa ni kitu ambacho hakitakiwi na hakizalishi vizuri, labda sehemu nyingine ambayo wameweka wakaleta utaratibu mzuri zaidi, wakafanye utafiti, kwa utafiti uliopo sasa hivi haina matokeo mazuri na mimi ni mkulima ninayesema hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaweza ikatoboreshea Minjingu lakini ituwahakikishie iweke subsidy kidogo, iwekwe kwenye soko ilete ushindani na mbolea halafu baada ya miaka miwili, mitatu wananchi wataamua wenyewe sio kuwala… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)