Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa na mimi nichengie japo kwa dakika tano katika hoja iliyopo mbele yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi niungane na wenzangu kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu pamoja na watendaji wote kwa kuandaa hotuba hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naomba nijielekeze moja kwa moja kwenye zao la biashara katika Mkoa wa Dodoma ambalo ni zao la zabibu. Katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri hakuna katika ukurasa wowote ambako amebainisha kwamba wanatoa kipaumbele gani katika kuendeleza zao la zabibu katika Mkoa wa Dodoma na hii inafahamika kabisa kwamba ni miongoni mwa mazao ambalo linaweza likawakomboa wananchi wa Dodoma katika suala zima la umaskini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nitaomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja kuhitimisha labda anieleze mkakati wa Serikali ni upi wa kuhakikisha kwamba zao hili linaweza likawekewa mkakati maalum. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna mbegu za kutosha kwa ajili ya zabibu, lakini sambamba na hilo mbegu za zabibu zinapatikana katika Kituo cha Makutupora. Kituo hiki bado hakina taasisi ya utafiti, kwa hiyo, hata baadhi ya magonjwa ya zabibu hayajulikani. Kwa hiyo, nilikuwa naomba niishauri Serikali yangu tukufu kwamba iione umuhimu wa kuanzisha kituo cha utafiti wa zao la zabibu ili kusudi kuweza kufahamu magonjwa na jinsi gani ya kuweza kupata suluhu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri ukurasa wa 38 amezungumzia kuhusu Sheria ya Zana za Kilimo. Naomba tu nihamasishe kwamba Serikali imechelewa kuleta sheria hii, hivyo basi hebu ifanye haraka kwani hizi zana za kilimo kwa kweli kuna baadhi ambazo hazikuwa katika ubora. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie pia kuhusu suala zima la alizeti. Mkoa wa Dodoma ni miongoni mwa mikoa ambayo mvua zake ni chache kwa hiyo mtawanyiko wa mvua ni kidogo. Kwa hiyo, zao la alizeti pia linastahimili katika Mkoa wa Dodoma. (Makofi)

Sambamba na hilo kuna changamoto nyingi, mbegu hazitoshelezi na wakulima wengi wanatumia mbegu ambazo wanakuwa wamezizalisha katika kipindi kilichopita. Kwa hiyo, nilikuwa naomba tu nitoe shime kwa Serikali yangu ione ni jinsi gani itaweka utaratibu wa kuhakikisha kwamba mbegu za alizeti zinapatikana kwa wakati na zilizo bora ili kusudi tuweze kupata hizo mbegu bora na hatimaye wakulima wetu waweze kupata mazao yenye tija.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, ninaunga mkono hoja.