Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Justin Joseph Monko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. JUSTIN J. MONKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia katika wizara hii muhimu kabisa ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri anaonesha kabisa kwamba asilimia 65.5 ya wananchi wa Tanzania wanashughulika na kilimo. Ukiangalia katika bajeti ambayo inaombwa na Wizara hii ni ndogo sana ukilinganisha na idadi ya Watanzania hawa. Watanzania hawa ndio ambao tumewaita katika hotuba hii kwamba ni maskini sana. Watanzania hawa ndio ambao wamekuwa wakihangaika kwa muda mrefu na kwa wakati wote huu tumekuwa tukiwatengea fedha kidogo kama ambavyo imeoneshwa katika takwimu. Nisingependa kurejea katika takwimu zilizopo kwa sababu ya muda ambao nimeupata katika kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mkoa wetu wa Singida na hususan Jimbo la Singida Kaskazini sisi ni wakulima wa vitunguu na alizeti. Katika taarifa ya Kamati mtaona kwamba nchi yetu inatumia fedha zaidi ya shilingi bilioni 413 kila mwaka katika kuagiza mafuta, lakini hatujaweka mkazo katika zao la alizeti ambalo linalimwa na wananchi wa Mkoa wa Singida na maeneo mengine. Ni kwa nini Serikali imeendelea kutoa fedha za kuagiza mafuta ghafi kwa asilimia 70 badala ya kuwekeza katika kilimo cha alizeti ili wananchi waweze kupata ajira? Kilimo ndicho kinachoajiri idadi kubwa ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais amepita katika maeneo mengi akisema yeye ni Rais wa wanyonge, wanyonge wa Tanzania hii wapo katika sekta ya kilimo huko vijijini. Ukienda katika majimbo yale ya vijijini zaidi ya asilimia 90 ya wananchi hawa wanategemea kilimo.


Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunahitaji kuwekeza sana katika kilimo ili kuweza kuwakomboa wananchi hawa ambao wamekuwa wanashinda kwa muda mrefu na kwa kweli hawapati fedha za kuweza kuendesha maisha yao, wameendelea kuwa maskini kwa muda mrefu kwa miaka mingi tangu tumepata uhuru. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niseme ukuaji wa sekta ya kilimo ni mdogo sana kama alivyoeleza Mheshimiwa Waziri katika hotuba yake. Mpaka sasa ni asilimia 3.1; hatuzuiliwi kwenda kwenye asilimia sita kama ukuaji wa uchumi ulivyo, tunahitaji kuwekeza fedha katika sekta hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.