Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi kutoa mchango wa sekta muhimu sana katika maisha yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaanza kutoa mchango wangu, naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia sisi sote na mimi mwenyewe binafsi angalau leo natoa mchango katika sekta hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wengi wamezungumzia umuhimu wa sekta hii, ni kwamba asilimia 75 ya Watanzania tuko vijijini na wengi walioko vijijini shughuli kubwa kule ni kilimo. Ukiangalia uchambuzi wa Kamati ya Kilimo, imebainisha wazi kabisa kwamba kasi ya sekta ya kilimo inazidi kuanguka mwaka hadi mwaka. Tunaiomba Serikali na maelekezo ambayo wametoa Wabunge waliotangulia, hebu muangalie changamoto hasa na baadaye mzipatie ufumbuzi wa kudumu katika kuendeleza hii sekta ya kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naungana mkono na Kamati ya Kilimo ambayo wameitaka Serikali kutambua fursa zilizoko na hizo fursa ambazo zinatambuliwa ndiyo mkakati hasa ufanyike. Mimi nitatoa mfano Mkoa wa Morogoro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wengi tunafahamu Mkoa wa Morogoro ni mkoa ambao tayari kuna miradi ambayo inaendelezwa pale. Naomba Serikali itupe mrejesho, kuna Mradi wa SAGCOT, kuna Mradi wa Feed the Future ambao unafadhiliwa na Wamarekani na vilevile kuna mkakati wa Fanya Mkoa wa Morogoro kuwa Ghala la Chakula lakini sii tunaotoka Mkoa wa Morogoro hatuoni jitihada za dhati kabisa juu ya miradi hiyo. Ukienda pale Morogoro, ukiuliza mtu wa kawaida tu SAGCOT unaijua, hawaelewi hali kadhalika hata huo mradi ambao unafadhiliwa na Marekani. Picha ya hapa ni nini? Kama kweli fursa zilizopo katika Mkoa wa Morogoro Serikali inawekeza pale, tunaweza tukatoa matokeo makubwa sana katika suala hili hasa la vyakula. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nijikite zaidi ili unielewe, mfano nitautolea Wilaya ya Malinyi. Wilaya ya Malinyi kama itawezeshwa kilimo cha umwagiliaji tayari pale kuna mito zaidi ya 30 inamiminika kuanzia masika na kiangazi, lakini wilaya yote ile kuna banio moja tu liko Itete.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeeleza mara nyingi na kuishauri Serikali, mnaonaje sasa mito mingine kwa mfano, Rasesa, Furua na Sofi, kama itatumika na kuweka scheme za umwagiliaji, nina uhakika tatizo la chakula litakuwa limetoweka kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakulima wa maeneo yale, wengi tunalima kilimo cha zao la mpunga na mahindi. Katika msimu wa mwaka uliopita tumechelewa kuanza kilimo cha mahindi kwa sababu ya shambulio la panya. Nilichogundua kwamba hakuna mawasiliano kati ya Wizara na watendaji walioko kule wilayani hawa Maafisa Ugani, vilevile kati ya Wizara na wananchi. Wadudu/panya hawa kumbe dawa yake ipo na dawa zinafanyiwa utafiti mara kwa mara kwenye Chuo cha SUA, SUA ndiyo center ya panya katika nchi hii. SUA iko Mkoa wa Morogoro, ni karibu sana na Malinyi, sasa kwa nini ndani ya miaka miwili mfululizo Wilaya za Kilombero, Ulanga na Malinyi tumekuwa na tatizo la panya lakini majibu hakuna! Kama mwenendo huu utaendelea, wananchi hawa wataendelea kuteseka zaidi na zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mbegu; wananchi Mkoa wa Morogoro pamoja na SUA tuna Kituo cha Utafiti cha KATRIN Ifakara, pale wanatengeneza mbegu ya kisasa ya SARO 5 lakini usambazaji wake wananchi mpaka leo hawaelewi. Kwa hiyo, hoja yangu hapa, namshauri Waziri, hebu uweke mikakati ya mawasiliano, mnafanya kazi nzuri pamoja na vyuo vyenu vya utafiti, lakini hakuna mrejesho kwa wananchi. Wananchi mpaka leo hawajui ni mbegu gani bora ya kutumia katika zao la mpunga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mara kadhaa nimeiomba Serikali kwamba wakulima wa mpunga wanasumbuliwa na ugonjwa ambao wa virusi. Ugonjwa huu kule tunaita kimyanga kwa lugha ya nyumbani, lakini lugha ya kitaalam unaitwa rice yellow mottle virus. Ugonjwa huu sio mgeni sana kwa nchi za Afrika, unapatikana sana West Africa. Niwaombe mara nyingine, kwa nini msipeleke wataalam waende wajifunze kule West Africa, wenzetu wameutatuaje ugonjwa huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu wa mwisho niongelee suala la masoko, wengi wameeleza, kama hatuna uhakika wa masoko kwa wakulima wetu kwa kweli tunapoteza nguvu za wakulima hawa. Niombe hasa soko la mpunga, mwaka wa fedha uliopita Serikali walitenga
angalau fedha za kuanza kununua karibuni tani 100,000 kupitia NFRA lakini naona kwenye bajeti hii wamesahau kabisa. Kwa hiyo, mtakapoweka soko hili la kupitia NFRA tayari itakuwa mmewatengenezea mazingira ya kuwa na soko la uhakika la zao la mpunga wananchi wale wa Malinyi, Kilombero na Ulanga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie la mwisho na niendelee kusisitiza tu, kama tunataka tutoke na kilimo chenye tija, twende na kilimo cha kibiashara ambapo sifa kubwa ya kilimo cha biashara inahitaji maji. Maji yapo, ni utaratibu namna gani tunaweza tukayatengenezea skimu tukayapata. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine tunataka miundombinu, kwa mfano kule Malinyi inafikia wakati bei ya mpunga inateremka na wananchi wanaumia kwa sababu miundombinu hali siyo nzuri sana. Mtu utoe gunia la mpunga pale upeleke kwenye soko Ifakara toka Malinyi ni kilometa 150 lakini gunia lile linagharimu shilingi 10,000 kwa gunia moja la kilo 100. Kwa hiyo, hii linampunguzia mapato huyu mkulima na matokeo yake hata soko sasa linapungua kwa sababu ya bei.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzangu wengine wamekuwa wanaeleza hawana imani na Waziri, mimi binafsi Mheshimiwa Tizeba namfahamu, uwezo wake ni mkubwa, naomba tumuunge mkono, tumtengenezee mazingira hata sisi Wabunge, huu ndiyo wakati wetu kutengeneza bajeti hii, kama ina upungufu, Kamati ya Bajeti ikaeā€¦

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)