Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee alikoishia mchangiaji aliyepita kwamba bajeti hii Serikali inyoongozwa na Chama cha Mapinduzi mmepoteana na Ilani ya Chama chenu lakini siyo tu kupoteana, mmepoteana na wapiga kura asilimia 80, waliowapigia kura ambao mnawaita ni wanyonge kila siku. Mheshimikwa Rais akisimama anasema Serikali ya Mheshimiwa Magufuli ni ya wanyonge. (Makofi)

Sasa kama ni ya wanyonge halafu bajeti ya wanyonge inapunguzwa kwa asilimia 34 bajeti ya development ya ajabu! Wanyonge gani wa nchi hii mnawaongoza wakati juzi tu kwenye maji mlipeleka asilimia 22, mkapitisha ile bajeti kwa caucus mkaitana mkaipitisha, lakini hii bajeti Mheshimiwa Waziri asilimia 18 tu ndiyo imepelekwa mpaka sasa, halafu mnajiita Serikali ya wanyonge, mlishapoteana zamani sana, siyo kupoteana na Ilani mpaka na wapiga kura. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mbaazi amesema Mheshimiwa Nape, Waziri kwenye kitabu chako mbaazi hata kuongelea ujaongelea kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hali ya kawaida Mheshimiwa Waziri hata mbaazi hujaongelea kwenye kitabu chako, maana yake unatuambia watu wa Kanda hii yote tuliyolima mbaazi tukale na watoto wetu ndiyo Serikali ya wanyonge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa natafuta kwenye kamusi nini maana ya laana, lakini nikaona tu niipotezee kwa sababu wakulima wa nchi hii wanawalaani sana maana wamekaa mazao yao, wamekaa na mbaazi zao na mahindi yao ninyi hamuhangaiki, unakuja hata huongelei suala la mbaazi Mheshimiwa Waziri, sasa unasema ni Serikali ya wanyonge asilimia 80 ya Watanzania hata huhitaji kuongelea? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mahindi mmesema hivi mnataka muongeze production ifike tani milioni nane kutoka tani milioni sita iliyoko sasa, lakini Mheshimiwa Waziri unafahamu mliunda Bodi ya Mazao Mchanganyiko, ile bodi wanahangaika mmewakabidhi tu majengo ya National Milling mpaka leo Bodi ya Mazao Mchanganyiko wanaomba shilingi bilioni tisa kwenu hamjawahi kuwapatia hizo shilingi bilioni tisa, hao watu bodi ya mazao mchanganyiko wangetusaidia kununua mahindi yetu, mbaazi zetu wakachakata. Mnaita Tanzania ya viwanda mmeshindwa hata kufufua majengo ya National Milling mpaka leo. Bodi ya Mazao Mchanganyiko wanaomba shilingi bilioni tisa kwanye bajeti mnawanyima, wameomba mkopo NSSF shilingi bilioni tatu hata Serikali haitaki ku-endorse huo mkopo halafu mnasema mna mkakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri kwenye kitabu chako umesema eti mmefungua mipaka mahindi yapelekwe nje ya nchi, huku mnasema kwamba ninyi ni Serikali ambayo inafufua viwanda na nchi ya viwanda hivi viwanda ndiyo kupeleka mazao nje ya nchi? Kwa nini
hamtaki kutoa hizi fedha shilingi bilioni tisa National Milling hawa na Bodi ya Mazao Mchanganyiko wakachukua mahindi yetu wakaweza kuyachakata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aibu zaidi katika Serikali yenu hii NFRA mliwapa fedha mwaka jana za kununua tani 18,000; mwaka huu mmewatengea fedha kununua tani 28,000 wakati mahindi tunazalisha tani milioni sita! Ninyi watu mmeshapoteana zamani sana, you are in the middle of nowhere! Hamjuani katika hili la wakulima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, inaudhi mimi naomba niende kwenye solution naipongeza sana Kamati hii na hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani ambayo wameshauri solution mbalimbali... (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)