Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Rashid Mohamed Chuachua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. RASHID M. CHUACHUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na mimi kupata nafasi ya kuzungumza kidogo kuhusiana na Wizara hii muhimu kwa uchumi wa Taifa letu, Wizara ya Kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuwapongeza sana Serikali pamoja na Mawaziri kwa kazi wanayoifanya kwa sababu changamoto katika kilimo zipo lakini yapo mambo ambayo hata wakulima wa korosho tunaona wameyafanya katika kupiga hatua mbele ya kutetea wakulima wetu. Changamoto zipo nasema lakini yapo mambo ambayo yamefanyika niwapongeze sana katika hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, asilimia 80 ya chakula kinachozalishwa Sub-Saharan African pamoja na Asia kinazalishwa na wakulima wadogo wadogo ambao wanatengeneza ajira takribani kwa watu bilioni mbili. Sambamba na hilo asilimia zaidi ya 70 ya watu wanaoishi kwenye Bara la Afrika ni wakulima wadogo wadogo, Tanzania tuna asilimia zaidi ya 60 ya wakulima wadogo wadogo. Hakuna ubishi kwamba this is the largest private sector on earth, lazima Serikali iangalie namna ya kutetea, kuwasimamia na kuwasaidia wakulima wadogo wadogo. Hata mjadala wetu katika Bunge kuanzia jana unawagusa wakulima wadogo wadogo. Ni muhimu Serikali sasa iangalie namna ambavyo inajikita sawasawa katika kupunguza au kuondoa kero zinazowakabili wakulima wadogo wadogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunao utaratibu unaosemekana wa kuanzishwa kwa mabenki kwa ajili ya kuwakopesha wakulima wetu, ukweli unabaki pale pale kwamba wakulima hawa hawakopesheki. Inawezekana hawakopesheki kwa sababu miundombinu yetu ya kisera, kwenye sera ya kilimo au sera ya fedha lakini inawezekana hii inatokana na sababu ya miundombinu ya utaratibu mzima wa kuangalia namna gani mabenki haya yanaweza yakawa- favor wakulima wetu haijakaa sawa. Tunahitaji kubadilisha taratibu zetu za kifedha au sera zetu ili wakulima hawa waweze kukopesheka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, umefika wakati wa Serikali kuangalia kwa kina ni namna gani inaweza kusimamia matumizi bora ya ardhi zetu. Ukweli uko wazi kabisa kwamba Tanzania ina ardhi kubwa, lakini yapo maeneo ambayo yanakabili sawa wakulima wadogo wadogo kutokana na kuingiliana na wafugaji kwa ajili ya migogoro inayotokea hapa na pale. Migogoro ya ardhi pamoja na migogoro ya vyanzo vya maji haya ni maeneo ambayo Serikali inatakiwa ichukue hatua ili mkulima aweze kufanya kazi yake kwa tiza zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati sasa umekwishafika kwa ajili ya Serikali kuangalia namna ambavyo wakulima wanaweza wakawa na bima katika shughuli zake za kilimo, hili ni jambo la muhimu sana. Ni jambo muhimu kuanzia mkulima anakwenda kuandaa shamba mpaka anapeleka mazao yake sokoni. Kwa sababu tunapoweza kuangalia mnyonyoro mzima wa thamani ndivyo tunavyoweza kuboresha maisha ya mkulima kwa kupunguza athari au risk inayoweza kumpata katika shughuli zake za kilimo. Haya ni mambo ambayo ni ya muhimu Serikali yetu ya Awamu ya Tano iangalie ili kuimarisha wakulima wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lipo pia eneo lingine, kilimo cha sasa lazima kiende sambamba na kisukumwe na haja ya soko la ndani na soko la nje. Ni lazima wakulima wetu wasimamiwe vizuri kabisa, namna gani wanaweza wakafanya kilimo chao kuwa biashara, wakati huo huo Serikali iangalie namna ya kupanua soko la ndani. Wabunge wengine wamekwishazungumza kwamba ili kutengeneza soko la ndani liwe na fursa ya kutosha ni lazima tuangalie namna ambavyo tunapanua uwekezaji katika viwanda vyetu ili Serikali iweze kuona namna gani wakulima wanaweza kuuza raw materials kwenye viwanda, wakati mnafikiria soko la nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, soko la nje ni muhimu kwa sababu tunahitaji fedha za kigeni, lakini soko la ndani ni muhimu zaidi kwa sababu tunahitaji wakulima hawa waweze kupata soko la uhakika. Leo hii tunauza asilimia zaidi 95 nje ya nchi. Leo hii tunauza pamba zaidi ya asilimia 80 nje ya nchi, hivi Wahindi ambao kwa mfano ambao ni wanunuzi wakubwa wa korosho pamoja Vietnam, wakisema sasa korosho ambazo wanalima huko zinawatosheleza tutauza wapi hizi korosho? Kwa hiyo, ni muhimu kuimarisha viwanda vyetu vya ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye masuala mengine ambayo Wabunge wameyazungumzia kwa kina. Mwaka huu Serikali kupitia Bodi ya Korosho ilifanya kazi ya kuingia mikataba na vikundi vya ujasiriamali pamoja na watu binafsi kwa ajili ya kuzalisha miche ya korosho. Katika mikataba ile Serikali iliwaahidi kuwalipa asilimia 30 kabla ya kuanza kufanya kazi na baadae kumalizia asilimia 70 ya malipo yao ili waweze kusambaza miche ya korosho. Ile advance payment haijalipwa, lakini kwa bahati mbaya sana mpaka leo hao waliosambaza miche kwa ajili ya mikorosho nao hawajalipwa. Hili ni jambo serious sana, kwa sababu ikiwa kila ambao wanajitolea na wanaonyesha uzalendo wa kusaidia sekta hii ya kilimo wanachelewa sana kulipwa fedha zao, utafika wakati watu wataona Serikali yetu haiko serious katika kuhakikisha kwamba wakulima wanapata huduma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lipo jambo lingine la muhimu na wengine wamekuwa wakilisema, mwaka 2015/2016 walitokea watu ambao walikuwa wanasambaza pembejeo mawakala. Hili jambo kila Mbunge amekuwa akilisema na mimi nasema umefika wakati sasa unajua ukiwaona hawa mawakala wako very loyal na wanaonesha kabisa kwamba fedha ambazo wanaambiwa na Serikali ndizo zinadaiwa kama deni siyo fedha sahihi. Inaonekana kwamba ni bilioni 35 tu ambazo ziliidhinishwa lakini ukizungumza na mawakala wanaonyesha wazi kabisa kuna vocha zilibaki na zilirudishwa kutoka katika Mikoa hawajui vocha hizi ziko wapi? Deni linaonekana ni shilingi bilioni 64, ukweli ni kwamba madai ya mawakala wetu ni tofauti na fedha zilizoandikwa na watendaji waliosimamia zoezi hili.

Kwa hiyo, ni aibu sana miaka karibu miaka mitatu, minne tunazungumzia tunawahakiki, tunawahakiki kitu gani? Wale walioiba tunawafahamu tukamate tuweke ndani na hawa watu wengine walipwe. Hili ni jambo muhimu sana ambalo tunapaswa kuliangalia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine mpaka leo wananchi wangu wa Masasi wameniagiza sana niseme sulphur haijafika na ile ambayo inauzwa kwa bei ambazo siyo rasmi na siyo halali zinauzwa zaidi ya shilingi 70,000 kwa mfuko mmoja. Ni lazima sasa Serikali...(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)