Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote kwanza napenda nimshukuru Mwenyezi Mungu aliyenijaalia kusimama katika Bunge hili kuweza kutoa mchango wangu katika hii Wizara muhimu kama tunavyofahamu kwamba Wizara ya Kilimo ndiyo Wizara muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, msimu wa mwaka 2016/2017 nilisimama kwenye Bunge hili, niliipongeza Serikali kupitia mfumo mzuri wa stakabadhi ghalani. Nilithubutu kusema kwamba mimi ni miongoni mwa waumini wa mfumo huu wa stakabadhi ghalani, ninaamini ni mfumo pekee ambao utaweza kumkomboa mkulima wa korosho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilieleza pia changamoto zilizopo kupitia mfumo huu wa stakabadhi ghalani. Mfumo huu wa stakabadhi ghalani, miongoni mwa changamoto zilizopo ni pamoja na wananchi kutokulipwa pesa zao kwa wakati. Waheshimiwa Wabunge wengi wamelizungumza jambo hili na katika vikao vilivyopita tulisema kwamba wananchi hawa wanapolima korosho na mazao mengine tumaini lao ni kutatua matatizo yao ikiwemo kusomesha watoto wao na mambo mengine mengi hata ikiwezekana kwa wale wababa ambao wanakusudia kuongeza wake wengine kupitia pesa hizi, lakini kinyume chake kimekuwa sivyo, wananchi wengi wamekuwa wakipata misukosuko. Sheria inaeleza kwamba baada ya kuuza korosho ndani ya siku saba mkulima anatakiwa apate pesa zake, lakini imekuwa sivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka hivi tunavyozungumza wapo wakulima ambao wanaendelea kudai pesa zao. Sisi Wilaya yetu ya Tunduru zaidi ya shilingi milioni 200 wakulima wanadai, inawezekana pengine kupitia udhaifu wa makarani waliopo katika vyama vyetu vya msingi na ninapozungumza makarani waliopo kwenye vyama vya msingi naamini kwamba taasisi hii inahusika moja kwa moja na ushirika, lakini inahusika moja kwa moja na Wizara ya Kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napata shida sana kwenye jambo hili kwa sababu mara nyingi tumelizungumza hapa kuona umuhimu wa wananchi kupata pesa zao. Sasa niombe Waziri atakapofika atueleze ni lini sasa wananchi wale watapata hizi pesa kwa sababu tumewahamasisha waweze kuuza mazao yao kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani, lakini badala yake imekuwa matatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na kutolipwa pesa na wakati, liko jambo lingine ambalo limejitokeza, wananchi kupata malipo yao kupitia benki, sina uhakika kama ni jambo la kisheria. Ninaweza nikazungumza upande wa korosho lakini baharti nzuri wako Wabunge wengine wamezungumza hata kupitia mazao mengine. Inaonekana kama ni jambo la lazima kwamba wananchi wapate pesa zao kupitia benki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, inawezekana Serikali ilikuwa na nia njema katika kuona fedha za wananchi zinabaki katika mikono salama, lakini badala yake imekuwa sivyo. Wakati wa mauzo ya korosho ukija Wilaya ambazo zinahusika na mazao haya utawahurumia wananchi. Wanapanga foleni kwenye mabenki, mtu anatoka kilometa 100 anakuja Makao Makuu ya Wilaya kufuata pesa yake, anakuja anaweza akakaa wiki nzima lakini anapofika dirishani anaambiwa pesa yako wewe haijaingizwa kwenye akaunti yako, mkulima yule anarudi kijijini, anarudi tena mjini imekuwa usumbufu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, zaidi ya hilo basi tutofautishe kwa sababu siyo wakulima wote ambao wanapata mazao kwa kiwango kinachofanana, wako wakulima wengine wanauza mazao yao kwa uchache kadri ya Mwenyezi Mungu alivyomjalia kuvuna, sasa tunamtaka hata mtu wa kilo tano aende akapokelee pesa zake benki, mtu wa kilo 50 aende akapokelee pesa zake benki, mtu wa kilo 100 aende akapokelee pesa zake benki.

Mimi naomba kama ni jambo la kisheria basi ni vizuri tufanye marekebisho. Wananchi hawa wanakata tamaa na huu mfumo. Inafika mahali wanaona kwamba siyo mfumo mkombozi, kwa hiyo mimi niombe na nimuombe Mheshimiwa Waziri ni vizuri kama ni jambo la kisheria na sheria hiyo iwe imetungwa na Bunge hili walete tufanye mabadiliko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwamba dhamira kubwa ya hawa wakulima wanapolima ni kutatua matatizo yao. Mtu ameuza korosho toka mwezi Novemba mpaka leo hajapata pesa yake, naliongea jambo hili kwa masikitiko makubwa na mimi ni sehemu ya wakulima wa korosho inauma sana, naomba Serikali ilitilie mkazo jambo hili katika kufanya marekebisho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nizungumzie suala la viuatilifu ikiwemo mbolea na sulphur. Wabunge wengi wamezungumza kuhusiana na suala la upatikanaji wa mbolea, tumekuwa tukisema sana, mbolea hizi haziji kwa wakati lakini leo tumepunguza ruzuku. Ukija kwenye sulphur, mwaka jana mimi nilisimama hapa kuchangia wakati tunasema kwamba Serikali itatoa sulphur bure, tuliipongeza Serikali, lakini tuliwaomba ni vizuri muweke mfumo sahihi ambao utaelekeza ni namna gani wananchi hawa watapata sulphur bure, leo mmekuja na mabadiliko mengine, hivi kweli tuna nia ya kuliendeleza zao la korosho kama siyo nia ya kuliharibu zao la korosho? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nilizungumze hili kwa sababu sote tumehamasika sasa hivi na ndiyo maana Waziri husika amefika mahali amepeleka miche ya korosho maeneo ambayo ana uhakika hata korosho hazitaota Wabunge wamesema hapa, ni kwa kuona korosho zimeongeza pato la Taifa letu, ni jambo jema lakini kwa nini tusisimamie tukaona hivi viuatilifu vinapatikana kwa wakati? Hii sulphur tumeeleza kwenye kitabu cha Waziri katika ukurasa wa 30 kwamba sulphur wanetegemea kwamba Bodi ya Korosho itatangaza bei. Hivi tunavyozungumza tayari korosho zimeanza kuchipua lakini mpaka leo bado…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)