Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Kilimo

Hon. Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Kilimo

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nami namshukuru Mungu kwa kupata nafasi ya kuchangia Wizara hii ya Kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya Wizara hii ya Kilimo kusema ukweli ni ndogo sana. Ukiangalia nchi yetu ni ya wakulima na wafanyakazi na haya makundi mawili asilimia 80 ni wakulima lakini bajeti inayotengwa hapa ni asilimia 4.8. Kusema ukweli hii asilimia haikidhi kabisa mahitaji ya wakulima hapa nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbolea pia ni janga la kitaifa. Mbolea bei yake ni kubwa sana ukilinganisha na hali halisi ya wakulima wetu hapa nchini. Cha kushangaza mbolea hii hii haifiki kwa wakati. Kwa mfano, mkulima analima mazao yakishaota mbolea ya kupandia ndiyo inakuja, wakati tayari mkulima ameshalima mazao yake. Inapofika kipindi cha mkulima kuvuna mazao, mbolea ya kukuzia ndiyo inafika. Kwa hiyo, niishauri Serikali kwamba mawakala wawe wa maeneo yaleyale husika kwa sababu kama kijiji fulani kinajulikana kabisa, kama mkisema chagua wakala wao wenyewe wanajuana, kwa nini wasifanye utaratibu huu kuliko kuweka wale mawakala wanaochaguliwa na Serikali? Kusema ukweli hawa mawakala hawafanyi kazi bali ni wachakachuaji tu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa tuna upungufu wa mafuta hapa nchini. Kusema ukweli ni jambo la kushangaza na ni aibu kwa nchi yetu. Ukiangalia tuna wakulima wanaolima ufuta na alizeti, kwa nini tusiweke kipaumbele kwa wakulima hawa ili tuweze kuzalisha mafuta ya kutosha katika nchi yetu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia mazao kama mahindi mengi hufikia wakati huharibika, kwa nini tusitafute wataalam wakaweza kutengeneza mafuta ya mahindi? Hakuna mafuta mazuri sana kama mafuta ya mahindi na yanashindana na mafuta ya olive oil. Wewe mwenyewe unajua kabisa jinsi olive oil ilivyo ya bei ghali na mafuta ya mahindi ni hivyo hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaangalia viwanda vingi vinategemea sana kilimo. Kwa mfano, katika Mkoa wangu wa Mara Kiwanda cha MUTEX kilikuwa kinazalisha nguo zenye quality nzuri sana. Hata hivyo, sasa hivi wakulima wa Mkoa wa Mara hawalimi tena pamba kwani imekuwa ni janga la kitaifa kwa sababu mkulima atalima ataenda kuiuza wapi? Tuangalie namna ya kumfufua mkulima wa zao la pamba kwa sababu hivyo viwanda tunavyosema Tanzania ya viwanda tunategemea tutauza vitu gani katika hivyo viwanda au tutangeneza kitu gani katika viwanda? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tujitahidi sana kuwasaidia wakulima wetu katika nchi yetu kwa sababu tunategemea sana kilimo. Kama kweli tunategemea kilimo na kilimo kinatusaidia na tunavyoangalia kwamba kilimo ndiyo uti wa mgongo na asilimia kubwa kati yetu tumesomeshwa kutokana na kilimo walichofanya wazazi wetu sasa iweje leo hii tumdharau mkulima? Naomba tuweke kipaumbele kwa wakulima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine ni upatikanaji wa mikopo. Kusema ukweli tumemminya sana mkulima kwenye hili suala la mikopo. Tunatoa asilimia 2 tu unategemea mkulima itamsaidia kwa kitu gani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia hizi benki naomba zifike vijijini. Benki hizi mara nyingi ziko mijini, wakulima vijijini mnategemea kwamba auze mazao yake apate nauli, aende kukopa kule mjini kwa kutumia mazao hayo hayo, kusema ukweli ni kuwatesa hawa wakulima. Kwa kweli naomba tuamshe akili zetu, Mheshimiwa Waziri naomba mnisikilize, tuamshe akili zetu tuwaone na tuweke kipaumbele kwa wakulima, tuwasaidie wakulima hawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mazao hasa ya mahindi katika Mkoa wa Mara, kwa kweli limekuwa ni tatizo kubwa sana. Sasa hivi wakulima wengi wanalima mahindi kwa ajili ya chakula tu.