Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Naibu Spika, Ushirika wa Wafugaji (Ayalabe Dairy Cooperative Society) na Ayalabe SACCOS Wilayani Karatu ni vyama vyenye usajili na viliingia katika mgogoro mkubwa mwaka 2014 na Serikali imetumia muda mwingi na rasilimali nyingi kuutatua, lakini bila mafanikio.
Mheshimiwa Naibu Spika, ngazi mbalimbali zikiwemo: Afisa Ushirika Wilaya na Mkoa; Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Ushirika - Mei, 2015; na Mrajisi wa Vyama vya Ushirika – Aprili, 2015 walitoa ushauri kunusuru ushirika huo lakini viongozi na baadhi ya wanaushirika huo wameendelea kupuuza na kukaidi yote. Mali ya ushirika huo zimeendelea kuharibika na Halmashauri ya Wilaya ilitoa sh. 500,000,000/=.
Mhshimiwa Naibu Spika, tangu Machi, 2015, Naibu Waziri alipotembelea vyama hivyo, hakuna kinachoendelea hadi hivi sasa na vyama hivyo viko kinyume na sheria, kwa kuwa muda wa viongozi umeshakwisha. Mgogoro huu uko ofisini kwa Mrajisi wa Vyama vya Ushirika Tanzania ili atoe maamuzi au ushauri kulingana na sheria na kanuni za Vyama vya Ushirika. Namwomba Waziri wa Kilimo na Mifugo, achukue hatua stahiki sasa kabla mali za ushirika huo hazijapotea zote.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama kuna dhambi kubwa anafanyiwa mkulima ni kumfikishia mbegu wakati wa msimu wa kilimo/kupanda imeshapita.
Misimu ya kupanda inafahamika katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu. Kwa nini mbegu zinachelewa? Hatujasikia hatua iliyochukuliwa kwa uzembe huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, wakulima wetu wanajua aina ya mbegu inayofanya vizuri katika maeneo yao. Baadhi ya mawakala wamekuwa na tabia ya kupeleka mbegu zisizofaa, kwa mfano mbegu za mahindi za muda mrefu (miezi 3 - 4) kupelekwa katika maeneo yenye mvua haba. Maoni ya walengwa/wananchi yaheshimiwe na wapelekewe mbegu za uchaguzi wao.