Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Kilimo

Hon. Mariamu Ditopile Mzuzuri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Kilimo

MHE. MARIAM D. MZUZURI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kutoa mchango wangu. Natangulia kwa kusema kauli inayosema nitasema ukweli daima fitina kwangu mwiko. Naenda kuchangia ukweli siyo fitina wala majungu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa, napenda kuwapongeza viongozi wetu wakuu wawili: Rais wa nchi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli na Waziri Mkuu, wameonekana namna gani wana dhamira ya dhati kuwasaidia Watanzania. Katika ziara zake zote Mheshimiwa Rais lazima atatue matatizo ya wakulima, hata Waziri Mkuu tumeona akihangaika kwenye kahawa, korosho, tumbaku kwa kweli hawa viongozi wetu kwenye hili wanapaswa kupongezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri wa Kilimo Mheshimiwa Dkt. Tizeba ni swahiba wangu lakini leo naomba nimwambie uswahiba baina yangu mimi na yeye haujazidi uswahiba niliokuwa nao na wakulima wa nchi hii. Najua jasho wanalolitoa, najua jinsi gani wanavyojikwamua na mazingira magumu lakini wanataka kupatia uchumi wetu kipato kikubwa. Kwa hiyo, leo hii nasimama kwa niaba ya wakulima wangu wa Chubi, Chamwino, Dodoma Mjini, Kondoa, Chemba, Soya, kote naomba niongelee machungu yanayowapata na naongea kwa facts. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze na zao la mahindi. Tanzania ilishatoka kwenye kilimo cha subsistence, hatulimi mahindi kwa ajili ya chakula, tunalima mahindi kwa ajili ya biashara na chakula. Leo hii ripoti yake yeye mwenyewe inamsuta amesema tumezalisha zaidi ya asilimia 120, kwa hiyo, suala la yeye kulinda food security asiende kuwaumiza watu ambao tunawaambia walime kwa ajili ya biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi mwenyewe ni kijana ambaye ni mkulima, nina mwaka wa saba kwenye kilimo lakini I regret to say ni mwaka wa kwanza sijalima. Nina gunia 6,500 juzi nimetoka kuzitupa zimeoza, tunaelekea wapi? It is very simple, Mheshimiwa Tizeba anakwenda kushauri viongozi wetu wakuu anawalisha matangopori kwa nini? Leo hii tayari tuna ziada na kiada ya mahindi anaenda kuweka zuio la ku-export mahindi lakini anaruhusu mahindi yaingie basi si angeacha tuminyane wenyewe ndani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkulima hajaomba mbegu hasa sisi wa Kanda ya Kati, Dodoma tunalima katika hali ngumu, anasema ili kwa Mheshimiwa Musukuma wasife njaa atuumize sisi. Musukuma ana madini, ana ziwa kule anavua samaki, sisi tunategemea kilimo, kilimo chenyewe ni cha machungu kweli kweli hatupati lolote kutoka Serikalini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii mahindi yameoza hali ni mbaya, anajibu majibu kirahisi oh hao wachuuzi, kwani wachuuzi wanaenda kununua na mawe yale mahindi? Mkulima kitu chochote akishavuna, amekaa miezi saba anasubiria kitu chini ya ardhi hajui hatma yake, anavuna mahindi yeye anachotaka apate hela aendelee na maisha, alipie watoto ada, aweze kula, aweze kujitibu anasema simply wachuuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi mkiwasema wachuuzi ndiyo vijana wangu wengi wa hapa Dodoma wamejiajiri katika sekta hiyo na hawa ndiyo wa kuwasaidia. Hebu tutathmini leo hii exporters wangapi wana asili ya Kitanzania? Sasa kama hatutowashika hawa mkono kuwapandisha tutazidi tu kuwa na wale wageni ambao ndiyo wanapeleka mazao nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni-regret sana kwenye mahindi kwa kweli basi angalau ungesema tunakataza kutoa nje lakini tusiingize kutoka nje ya nchi. Leo hii Zambia wameingiza mahindi mengi Mtwara, Lindi mpaka Himo, mahindi yetu yamekwama hakuna soko, huo ndio ukweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja kwenye tumbaku, kwa sababu anajitetea sana Mheshimiwa Waziri. Uongozi una vitu viwili, sawa bajeti anapelekewa ndogo lakini kuna utashi, Waziri ana utashi gani, hapa umesoma hotuba yako hata hatujasisimkwa sisi kama wakulima. Bajeti ya kwanza aliongea Mheshimiwa Mwigulu hapa kila mtu alisisimka kama mkulima alisema kabisa sasa hivi yale mageti hakuna kuzuia magunia ya wakulima muwaache. Alienda kutatua kero ambayo inamgusa mkulima wa kawaida, but now nothing my friend, nothing. Sawa Waziri anapelekewa bajeti ndogo lakini utashi, ameaminiwa na Mheshimiwa Rais apeleke kilimo kwa ajili ya kuleta uchumi wa viwanda lakini ndiye yeye anavuruga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, world market price ya tumbaku, Cost, Insurance and Freight mpaka Vietnam ilikuwa kilo moja ni dola 2.20. Wanunuzi wetu hapa walikuwa tayari kwa sababu ununuzi wa tumbaku ni pre-order, walikuwa tayari kununua zaidi ya order waliyotaka lakini wakaomba wanunue kwa dola 1.3 lakini Mheshimiwa Waziri akakataa huku akijinadi kwamba ana wanunuzi. Akaenda nasema tena tangopori akamlisha Mkuu, akamlisha Mheshimiwa Waziri Mkuu lakini Wabunge wa Tabora huku walichachamaa wakasema mbona wanunuzi wanazuiwa kununua na tumbaku zinakaa muda mrefu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumbe inavyosemekana Waziri alisema kwamba wanataka kununua kwenye 0.8 lakini ilikuwa wanataka kununua kwa 1.3. Kilichotokea mvua imenyesha, hawana vihenge wale, hawana sehemu ya kuhifadhia, wanalima ili wauze waweze kuendelea na maisha mengine, tumbaku zimeharibika, zimeshuka thamani, mwisho wa siku wameuza kwa 0.8 USD. Kwa hiyo, zile pesa walizopata wameenda kulipa tu madeni hakuna chochote yaani kwa kweli wenzangu Wabunge wa Tabora watakuja kusema hali halisi, mimi ni Mbunge wa nchi nzima kwa hiyo lazima niliongelee. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja kwenye korosho. Picha tunayoipata kwenye korosho kwa kweli niwaambieni siyo juhudi za Wizara, ni kudra ya Mwenyezi Mungu. Tuna advantage kwamba msimu unapoanza sisi ndiyo nchi ya kwanza ya kuvuna korosho, kwa hiyo, tunakuta makampuni mengi yanahitaji ile korosho. Ndiyo maana mpaka leo korosho ina bei ya juu tunapoona kwenye minada. Vilevile in the world Tandahimba, Newala, Masasi na Mtwara ndiyo ambao wana-produce korosho nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, I was in India, nilienda kuongea na watu kwa ajili ya kuwauzia korosho bahati mbaya niliharibu kwa sababu nilikuwa na rafiki yangu kutoka Ghana, wale waliniambia Ghana nao wana korosho nzuri but still virgin hawajagundua, basi maneno yale hayajaenda kushoto wala kulia, Ghana wamezindua Mpango wa Miaka Kumi wa Kunyanyua Kilimo cha Korosho, tusubiri tutakayoona, hatuna mipango endelevu. Bodi ya Korosho wanai-disturb, korosho ni zao la biashara, linaenda vizuri, linaleta mapato, ghafla unasema sulphur ipelekwe bure waliomba, ndiyo mahitaji ya wakulima? Mmeshindwa kuzifikisha kwa wakati korosho zikaingia magonjwa hakuna dawa ya kutibu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, magunia, minada imeanza, mtu ana korosho zake nyumbani hamna magunia na yaliyomo chini naomba vyombo vya ulinzi na usalama vikachunguze mnajua wenyewe. Haya leo hii wamerudi tena nyuma, kwa nini tuna-disturb industry? Wamerudi nyuma tena wanasema ooh sulphur hatuzitoi bure, mliombwa mtoe bure? Kwa nini mna-disturb wakulima na watu wanaenda katika njia nzuri? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mipango endelevu tuliyokuwa nayo leo hii badala ya kutoa korosho kama raw material tunaenda kuongeza miche. Mimi napenda kwamba kila sehemu tulime korosho kwa sababu it is a green gold lakini nilitoa hapa mchango mwaka wa kwanza nikasema tuweke agricultural zone, kila sehemu hapa ina zao lake, kwa nini tusikazanie huko? Unaniletea mikorosho Dodoma hakuna hata Afisa Kilimo mmoja aliyefundishwa utaalamu, hiyo mikorosho ikiota asilimia 10 najiuzulu Ubunge, iko majumbani imekauka. Unawapelekea watu hujawapa utaalam, tena system unayo, kuna Maafisa Ugani kila Kata na Kijiji, waite wape elimu halafu ndiyo usambaze, hamtoi elimu mnaenda kugawa mikorosho, tutaona mwisho wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hebu mimi niwashauri kidogo tu, tuweke mazingira mazuri, huwezi ukampa mazingira sawa mtu anaye-process korosho na yule anayeitoa nje, hebu tuwa-favor hawa. Kuna kitu kinaitwa opportunity cost ingieni.