Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Mwenyekiti, nalipongeza Jeshi la Ulinzi kwa kazi nzuri na ya kizalendo inayofanya kuhakikisha nchi yetu na mipaka yake ipo salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Tanzania kwa uongozi wake bora wa kulisimamia Jeshi letu la Tanzania. Nampongeza Waziri wa Ulinzi wa Jeshi la Kujenga Taifa, Watendaji wote wa Wizara na Wakuu wa Majeshi wote nchini kwa usimamizi wa majeshi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali ijitahidi kuongeza bajeti kwa Wizara hii kwa lengo la kuongeza ufanisi wa kazi zake na kutekeleza majukumu yake kwa wakati. Vile vile Wizara iongeze kuelimisha majeshi yetu katika vitengo vya uhandisi na teknolojia ya kisasa ili kukabiliana na changamoto mbalimbali za sayansi na teknolojia zinazojitokeza. Pia majeshi yetu kujitosheleza na wataalam hao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kambi za Jeshi zilizopo karibu na makazi ya raia au kuzungukwa na maeneo ya raia ziangaliwe ili yasije yakatokea madhara kwa raia wa maeneo hayo. Pia juhudi za Wizara za kuwapatia wanajeshi wetu makazi bora ziendelee kwa lengo la kuwapatia wanajeshi wetu maisha bora na yenye utulivu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.