Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, napenda kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Hussein A. Mwinyi, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa kazi nzuri anayoifanya katika Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali iongeze muda wa compulsory program kwa vijana wetu (mwaka mmoja), ili kuweza kuwajengea uwezo wa kujifunza mambo mbalimbali mfano; ujenzi, uashi, kilimo, ufugaji na kadhalika ili wamalizapo kuwa na uwezo wa kujiajiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali iwasaidie familia ya Wanajeshi wetu ambao mara nyingi hupoteza maisha wakiwa katika harakati za kulinda amani katika nchi za jirani mfano kuwasomesha watoto wa Marehemu, maana mara nyingi warithi wa familia hawawatendei haki watoto hao walioachwa na marehemu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuleta mahusiano mazuri baina ya wananchi na wanajeshi wetu, naishauri Serikali itoe elimu ya kutosha kwa Wanajeshi wetu wa Tanzania kutokuchukua sheria mikononi kwa wananchi wetu. Mara nyingi kuna matukio mengi yanatokea Wanajeshi kuwapiga wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali iboreshe maslahi ya Wanajeshi wetu, mishahara iongezwe ili waweze kufanya kazi kwa weledi, pia wajengewe nyumba bora na kupatiwa usafiri wa kuwapeleka makazini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali iboreshe makambi yetu ya kujenga Taifa hususani Mahanga (bweni) na maofisi maana majengo mengi ni ya muda mrefu na chakavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, namwombea Mheshimiwa Waziri Dkt. Hussein Ally Mwinyi kila la kheri, afya njema na umri mrefu ili aweze kuwatumikia Watanzania.