Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nafasi ya kipekee, naomba kuchukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Mkuu wa Majeshi na watendaji wote wa Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwapongeza sana sana wanajeshi wote walioshiriki katika operesheni ya Kibiti. Kazi hii waliyoifanya ilikuwa ni nzuri sana na ya kutukuka. Wanajeshi hawa wanastahili pongezi za dhati sana kwani walijitoa uhai wao kwa ajili ya Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua wanajeshi hawa walishalipwa stahili zao zote? Je, kiwango kilicholipwa kinafanana na kile cha wenzao wa TISS pamoja na Polisi? Nashauri Jeshi kuangalia na kufanya tathmini ya malipo yote waliyolipwa pamoja na stahili zao kama zilikuwa zinalingana na wenzao wa taasisi nyingine nilizozitaja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza lakini hili naomba lifanyiwe kazi. Ahsante sana.