Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu Kambi ya JKT iliyopo katika Kata ya Itaka Wilaya ya Mbozi, kuna migogoro ya mipaka ya ardhi na wananchi wa Vijiji vya Sasenga, Itewe na Mboji. Ramani ya vijiji hivi pamoja na GN vinaonesha kuwepo kwa vijiji hivyo miaka mingi kabla ya kuanzishwa kwa kambi ya JKT.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali ishughulikie migogoro ya mipaka kati ya JKT na vijiji hivi kwani kuchelewesha utatuzi wa migogoro kutasababisha uadui mkubwa kati ya wananchi na JKT jambo ambalo siyo jema. Kijiji cha Sasenga wananchi wameamuliwa wote kuhama ili kupisha maeneo ya jeshi bila kuwaonesha kwa kwenda ni uonevu mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Kujenga Taifa JKT liboreshe na kusimamia kwa ufanisi zoezi la kuwapata wananchi wa kujiunga na JKT kupitia wilaya zao. Mwaka jana Wilaya ya Mbozi wananchi walioomba kujiunga na JKT waliachwa wote na badala yake wakachukuliwa watu wa kutoka nje ya Mbozi na nje ya Mkoa wa Songwe. Naomba viongozi wa JKT toka Makao Makuu washuke hadi kwenye Wilaya kusimamia zoezi hili vizuri na wasiachiwe Wakuu wa Wilaya maana ndiyo chanzo cha migogoro na upendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia mishahara iongezwe kwa wanajeshi wetu maana wanafanya kazi nzuri ya kulinda mipaka ya nchi yetu. Makazi yao pia yaboreshwe maana hali ni mbaya sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.