Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja ya Bajeti ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Napongeza sana kwa namna ambavyo Jeshi letu linavyoendelea kuchapa kazi na kuendelea kuimarisha amani ya nchi yetu. Naliomba sana kuendelea kuyalinda maslahi ya Jeshi letu, lakini kujengewa mazingira mazuri ya kazi zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie Mkoani Lindi, Wilayani Nachingwea, tunayo Kambi kubwa ya Jeshi maarufu kama Majimaji camp. Kambi hii ni kubwa ilijengwa na Baba wa Taifa. Naomba sana Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kutembelea na kujionea hali halisi ilivyo pale, nyumba za Askari wetu zimekuwa chakavu sana na majengo pia yamekuwa machakavu. Naiomba Serikali kuboresha nyumba zile na majengo yao ya kazi ili waishi katika mazingira safi na rafiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja. Ahsante sana.