Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, narejea ukurasa wa 26 wa kitabu cha Mheshimiwa Waziri, ameeleza juu ya wanajeshi wa nchi yetu kupoteza maisha wakiwa katika jukumu la kulinda amani nchini DRC. Jambo hili la ulinzi ni jambo jema kwa nchi yetu kushirikiana na nchi nyingine. Napenda kuishauri Serikali yetu kwa kushirikiana na nchi za Afrika kushauri Umoja wa Mataifa ili kusaidia DRC kujenga jeshi liwe imara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi hii ina population ya zaidi ya milioni sitini, wana rasilimali za dhahabu, shaba, misitu na kadhalika. Ni kwa nini nchi hii imeshindwa kuunda jeshi lao na nchi zinapeleka askari na wanapoteza maisha? DRC imepigana tangu 1994 hadi leo. Nchi za Rwanda na Uganda na kadhalika zimepigana vita na wameondoa majeshi yao. Umoja wa Mataifa hutumia fedha nyingi, takribani bilioni moja Dola za Kimarekani kila mwaka kwa ajili ya matumizi ya majeshi almost 29,000. Fedha zinaweza kutumika kufundisha Jeshi la Congo kwa kusaidiana na majeshi yaliyopo. Nchi yetu inaweza kusaidia kutoa ushauri ili watoto wetu wasiendelee kuuawa huko DRC.