Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachangia bajeti hii kwa kupenda kujua na kuishauri Serikali kwamba katika Kikosi/Kambi ya JKT Chita, pamoja na kuwa na umuhimu wa uwepo wa kambi hiyo, ni muhimu kukawa na mpango wa ujirani mwema kati ya Chita JKT na Vijiji vya Makutano, Chita na Ikule kwa Kata ya Chita na Mngeta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni miaka mingi sasa wananchi wana malalamiko ya mipaka ambapo kuna wakati Jeshi kuingia hapo, hasa Kata na Kijiji cha Chita. Ingawa kwa upande wa pili Kata ya Mngeta hawakuwa na ombi lolote kwenye Kijiji cha Mkangawalo na kuleta sintofahamu inayojitokeza ambapo wananchi wanaomba kuwepo na maelewano kwa kuwa ni miaka kadhaa sasa hawana maeneo ya mashamba na kuwafanya kuwa maskini kwani tegemeo lao ni ardhi ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na mazungumzo ya ana kwa ana na Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi kuwa wananchi hao wataangaliwa kwa kuwafanya wakulima wadogo kwani kutafanyika ukulima mkubwa na SUMA JKT, lakini ni miaka sasa inapita hakuna mwananchi aliyeingizwa katika kilimo hicho. Serikali iwaonee huruma na wananchi hao wanaoteseka na kunyanyaswa katika maeneo hayo. Je, ni lini sasa Serikali itakaa na wananchi wa vijiji hivyo ili wananchi waweze kuwa na maeneo ya kilimo na kujikimu na hali ngumu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna wanajeshi wenye elimu ya kiwango cha chuo kikuu. Wakati wa Rais Kikwete (Operesheni Kikwete) waliorudishwa nyumbani wangefikiriwa kupata ajira lakini hadi leo hawajaitwa. Je, ni lini sasa Serikali itawakumbuka vijana hao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ione haja ya kupitia maeneo yote yanayolalamikiwa kwa kuwashirikisha wanavijiji na Jeshi na mamlaka zinazohusika ili kuleta utangamano.