Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, napongeza hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi na kazi zao wote kwa ujumla.
(i) Lini Chuo cha Uvuvi kilichokuwa kinazungumziwa kwenye Wilaya ya Nyasa kitaanza?
(ii) Kwa nini ushuru wa uvuvi unabadilika mara kwa mara kwa madai kuwa unachajiwa kwa dola kwa mujibu wa sheria? Je, ni kweli? Kama ni kweli, hiyo sheria itarekebishwa lini? Kwani ni mateso kwa wananchi.
(iii) Kuna malalamiko makubwa ya watumishi wa uvuvi ambao wapo katika forodha ya Mbambabay hususan Bwana Saleke. Nashauri mkamtumie sehemu nyingine kwa kubadilishwa kituo cha kazi.
(iv) Jimbo langu ni wakulima wa mihogo kama zao kuu la mwambao, tunaomba mbegu za kisasa kwa mfano za kiloba.
(v) Kwa kuwa eneo pia ni zuri kwa ndizi, tunaomba mafunzo ya kilimo cha ndizi.
(vi) Tunashukuru boti ya Doris, iongezwe moja kwa ajili ya Kituo cha Ng‟ombo hasa kwa ajili ya uokoaji.
(vii) Kahawa ipunguzwe ushuru. Naungana na Mheshimiwa Sixtus Mapunda, Mbunge wa Mbinga.
Hongereni na naomba kuwasilisha.