Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Dr. Philip Isdor Mpango

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Na mimi nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Naibu wake, Mheshimiwa Engineer Manyanya; timu nzima ya uongozi wa Wizara kwa kazi nzuri wanayoifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nisisitize kwamba viwanda ndiyo njia pekee ambayo ilifanya nchi zote ambazo tunaziita zimeendelea kuendelea. Kwa hiyo, hii ni njia sahihi, Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na timu nzima kazaneni, mkaze buti, hii ndiyo njia sahihi ya kwenda kadri ya uongozi wa Serikali yetu inavyotaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuchangia niseme mapema kabisa kwamba naunga mkono hoja na nitachangia kwa kutoa ufafanuzi wa mambo machache na mengine tutaendelea kuyafafanua kadri mjadala wa bajeti unavyoendelea mpaka huko mwishoni mwa mwezi Juni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza ambalo napenda kulitolea maelezo, pamekuwepo hoja hapa kwamba watu wanateseka sana kwa fedha zao ambazo zimekwama kwenye iliyokuwa benki ya FBME ambayo tuliiweka chini ya ufilisi. Naomba tu niseme kwamba Serikali inawajali watu wake na imekuwa inalishughulikia jambo hili inavyopaswa na kwa mujibu wa sheria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfilisi ambaye ni Deposit Insurance Board (DIB) imeendelea kulipa amana za wateja na tulianza hiyo kazi toka tarehe 1 Novemba, 2017. Mpaka kufikia tarehe 8 Mei zimeshalipwa shilingi bilioni 2.31 kwa kiwango kile cha juu ya shilingi milioni moja na nusu ambayo imefikia sasa takriban asilimia 53 kati ya shilingi bilioni 4.3 ambazo zilitarajiwa kuwa zimelipwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, waliolipwa ni wenye amana takribani 3,203 ambayo ni asilimia 48.1 ya wateja wa iliyokuwa hiyo benki. Malipo yalibaki tutaendelea kuyalipa, hususani yale ambayo yanahusu amana yatafanyika baada ya kuwa tumefanya uhakiki wa mikopo mbalimbali ya wadaiwa na madeni ya hiyo benki. Kwa hiyo, hilo naomba niliachie hapa kwa sasa, nikisisitiza tu kwamba Serikali inawajali wananchi wake na itahakikisha kwamba haki yao inapatikana baada ya taratibu kukamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa na suala la export levy ya ngozi. Sasa hili, ngozi ghafi ni muhimu sana. Ule uamuzi wa kuweka export levy ulikuwa ni wa makusudi. Ni lazima tulinde ajira, tuuze nje kile ambacho kimeongezewa thamani ndiyo wananchi wetu wataweza kufaidika. Tusipofanya hivyo, maana yake tunawapatia ajira huko ngozi zitakapokwenda. Kwa nini tufanye hivyo wakati tunalia na ajira ya vijana wetu?

Pia kulikuwa na hoja juu ya rai kwamba wafanyabiashara wetu wanapo-declare zile fedha kwenye mipaka, hali inakuwa ngumu kweli! It is very risk na wengine hata wanauawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Serikali ilivyoshauriwa, tutaendelea kuliangalia hili jambo la namna ambavyo watu wetu wana-declare fedha walizonazo pale mpakani. Napenda kutumia nafasi hii kuvitaka vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kuimarisha usalama katika maeneo yale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nitumie fursa hii kuikumbusha Mamlaka ya Mapato/watumishi wetu wa Mamlaka ya Mapato ni marufuku kutoa siri za wananchi/ wateja wetu wanapo-declare fedha zile. Nitumie nafasi hii kumwagiza Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato
kuandaa viapo vya watumishi wetu waliopo pale mipakani kuhakikisha kwamba atakayekiuka vile viapo, basi anapata habari yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nadhani ni muhimu niseme kwamba hatua hii ni muhimu kwa ajili ya kuzuia utakatishaji fedha, lakini hata ufadhili wa ugaidi. Kwa hiyo, hili jambo ni international practice na lazima na sisi tuendelee kufanya ili Taifa letu liendelee kuwa salama. Pia wananchi wenyewe husika ni muhimu wakachukua tahadhari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa na hoja ya Mamlaka ya Mapato kupuuza invoices za wateja na kuzikadiria upya. Kiini cha shida hii kwa kweli ni udanganyifu. Watu wanatoa value ya hizi invoices zisizo sahihi na ni kwa makusudi kwa sababu kama ingekuwa ni human error

unategemea kwamba basi invoice zilizozidishwa au zile zilizopunguzwa ziwiane, lakini daima sivyo, under invoicing ndiyo kubwa. Kwa hiyo, ni muhimu sana kwamba wananchi nao wanaohusika, wote tunawataka watoe invoices ambazo ni sahihi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa na hoja watumishi wetu wa TRA kudai rushwa. Hili napenda nitumie nafasi hii kulikemea kwa nguvu zote. Hili ni kosa kubwa na Serikali ya Awamu ya Tano imejitabanaisha kwa kupambana na rushwa. Kwa hiyo, nitumie nafasi hii kuwaomba Waheshimiwa Wabunge na wananchi ambao wanatusikiliza, watupatie taarifa pale ambapo pana mtumishi yeyote wa TRA ambaye anadai rushwa, nasi tutamtumbua, wala hatutanii. Tupatieni taarifa tutawafanyia kazi ipasavyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa na suala pia kuhusu research and development. Ni kweli tunapokwenda kujenga uchumi wa viwanda, research and development ni jambo la msingi sana. Rai yangu ni kwamba Watanzania tushikamane, tuendelee kukusanya mapato zaidi na zaidi kadri inavyowezekana na kupanua wigo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.