Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, zuio la mifuko ya plastic; nchi jirani zote katika kutekeleza the so called EAC Polytene Material Control Bill ilipitishwa baada ya muda wa karibu miaka mitano, zimezuia kabisa uzalishaji, usambazaji na matumzi ya mifuko ya plastic. Sisi Tanzania mpaka sasa tumeendelea kuzalisha mifuko ya plastic kwa namna ambayo imejaa ujanja mtupu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya Kenya na Uganda kuzuia, sasa sisi tumegeuzwa soko. Kati ya tani zaidi ya 1,500 zinazosambazwa kwa mwaka ni tani 100 tu ndo zinazalishwa hapa nchini, maana yake ni kuwa chini ya asilimia kumi ndio inazalishwa hapa nchini. Hivyo hoja ya kuwa tunalinda viwanda sio kweli kwa sababu asilimia 90 ya mifuko inatoka nje na zaidi nchi jirani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira wanasema Viwanda, Biashara na Uwekezaji ndio kikwazo, wao hawana tatizo. Ni matumaini yangu kuwa kwenye hitimisho, Wizara itakuja na maelezo ni kwa nini mpaka sasa haijazuia uzalishaji kama inavyodaiwa wa mifuko ya plastic?

Mheshimiwa Mwenyekiti, BRELA na usajili wa kimtandao; wananchi wengi siku za nyuma waliliwa fedha zao na middle men, lakini toka usajili kuanza kufanyika kwa njia mtandao (online) kumekuwa na ufanisi wa hali ya juu, ni suala la kupongeza, ushauri, BRELA ifanye semina nyingi kadri iwezavyo ili elimu hii ienee maeneo mengi hasa yenye uzalishaji, kwa mfano Mafinga ina shughuli nyingi za mazao ya misitu, kuna mbao lakini wengi wa wafanyabiashara bado hawana elimu ya kutosha kuhusu umuhimu wa kuwa na kampuni na faida zake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, michezo ya kubahatisha; hii ni biashara inayokuwa kwa kasi sana. Hata hivyo taratibu zinazotawala biashara hii hazileti matunda bora, kwa mfano ilivyo sasa katika Sports Betting, mchezeshaji analipa asilimia sita ya mauzo ghafi. Hii iliwekwa kwa ajili ya kuvutia wawekezaji, baada ya kukua kwa hii biashara, ni wakati sasa kuzingatia yafuatayo:-

(i) Kuonesha uhuru/kodi ya mauzo kutoka asilimia sita hadi asilimia 20. Maana yake katika kila shilingi 100 Serikali itapata shilingi 20 badala ya shilingi sita ilivyo sasa.

(ii) Ili kuvutia wachezaji wengi ambao sasa baadhi yao wameanza kupendelea kucheza Sports Betting za nje kwa hoja kuwa makato ya asilimia 14 ya zawadi ya mshindi ina-discourage. Ni afadhali kanuni ikawa kwa mfumo wa capital gain asilimia kumi. Hii itachochea wengi kucheza na Serikali kupata nyingi katika ile asilimia 20 ya mauzo ghafi maana washindi ambao hutupatia asilimia 18 ni wachache kuliko wachezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda vilivyobinafsishwa; ushauri wangu kama ambayo Serikali inatutajia idadi ya viwanda, ituambie status ya viwanda vilivyokuwa vimebinafsisha ikoje, vingapi vinazalisha na kwa capacity gani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda vya mazao ya misitu; nimeshaiomba Wizara na Waziri tufanye kongamano tukihusisha vyombo vyote muhimu kama vile BRELA, OSHA, TIC, TIB, TRA, TFS, NEMC na Wizara ili wawekezaji wa mazao ya misitu waweze kuelezwa fursa zilizopo, lakini pia kueleza changamoto wanazokabiliana nazo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya mazao ya misitu ni eneo lenye potential kubwa. Ni masikitiko yangu kuwa jitihada za kumuomba Waziri kutembelea Mafinga ili kujione uwekezaji lakini pia kujionea changamoto zinazowakabili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.