Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la vipimo, maduka yote yawe na mizani ya kupimia bidhaa zinazouzwa. Mizani hiyo iwe na uwezo wa kupima zaidi ya kilo 50 ili mteja akihitaji sukari ya kilo 50, cement ya kilo 50, unga wa ngano kilo 50, mbolea ya kilo 50 aweze kupimiwa, maduka mengi yanayouza bidhaa hizo hayapimi na kwa wafanyabiashara wasio waaminifu huwaibia wateja na kuwasababishia hasara wateja hao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namba za ubavuni kwenye malori ya mchanga Wizara iangalie viwango vya kuandika namba za ubavuni na hasa pale inapokuwa inaandikwa kwa mwaka wa pili, ada hii ni kero na haina uhalisia hivyo inasababisha maudhi na usumbufu kwa wamiliki wa magari hayo, nafahamu fika ni sheria na nia ni kumlinda mlaji, lakini

gharama za kuandika namba hizo inamrudia huyo huyo anayelindwa. Hivyo nashauri Serikali iondoe ada ya kuandika namba ya ujazo kwa mara ya pili ili kuondoa gharama na kero kwa wamiliki. Kama ipo kwenye sheria ya msingi basi iletwe Bungeni na kama ipo ndani ya uwezo wa Wizara basi jambo hili liangaliwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeshindwa kabisa kudhibiti rumbesa ya viazi mviringo, hii ni aibu kwa wataalam wa Wizara kushindwa kudhibiti jambo la wazi kama hili. Serikali isaidie ujenzi wa parking house (cold room) ambazo zitawasaidia wateja wa matunda aina ya parachichi kuweza kununua matunda hayo na kuyaandaa vizuri kwa ajili ya masoko ya nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kufanya hivyo utakuwa umewawezesha wakulima kuuza zao hili na kuisaidia nchi kupata fedha za kigeni kwani parachichi zinazolimwa Njombe zimepata soko nje ya nchi na hasa Ulaya.