Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, urasimu wa kupata leseni ya biashara; wafanyabiashara katika Halmashauri husika wanapata shida kupata leseni ya biashara kwa masharti ya kuwa na TIN number ya TRA. Akifika TRA anaambiwa lazima afanyiwe makadirio ya kodi ya biashara yake bila hata kuiona biashara yenyewe. TRA Officers wanakaa ofisini na kufanya makadirio ya mfanyabiashara bila kuona ukubwa wa biashara yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfanyabiashara akishakadiriwa kodi ya juu zaidi ya biashara yake anagoma kukata TIN, kisha anaendelea na biashara zake bila kuwa na leseni jambo linalopoteza mapato ya Halmashauri kwani leseni zinakatwa na Halmashauri baada ya kuwa mfanyabiashara amekidhi masharti ya TRA ya kuwa na TIN number.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri, TRA wasifanye makadirio ya kodi kwa wafanyabiashaa wakiwa ofisini, wafike site wakaone ili wasiwaonee au kuwapendelea wafanyabiashara. Leseni za biashara zitolewe na Halmashauri bila masharti ya kuwa na TIN number ili waendelee na biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uwekezaji, viwanda vikubwa na vya kati hutegemea nishati ya umeme. Kakonko hakuna umeme wa uhakika wa kuwavutia wawekezaji kuja kuweka viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda hutegemea miundombinu ya barabara kwa ajili ya kusafirisha malighafi, Kakonko hadi Kigoma ni kilometa 30 na barabara ni mbovu hivyo haiwavutii wawekezaji kuwekeza Mkoa wa Kigoma na Wilaya zake kama Kakonko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri aliahidi kiwanda cha kuchakata mihogo tangu mwaka 2016 na kiwanda hicho kinasubiriwa Kakonko. Nashauri kiwanda hicho kipatikane ili wananchi waendelee kuwa na imani naye asije kuonekana ni muongo. Heshima ya Kiongozi ni kutekelekeza ahadi zake anazotoa.