Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono, nawatakia kila la kheri katika utendaji mzuri uliotukuka. Naomba sana na kwa mara nyingine ulinusuru zao la pamba tumkomboe mkulima wa pamba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zao la pamba linaonekana kama zao lisilokuwa na maana, ili kuwakomboa wakulima wa pamba, naomba Nyambiti Ginnery ifufuliwe ili ianze kazi ya kuchambua pamba kama ilivyokuwa zamani. Tathmini tayari imeshafanyika kupitia mifuko ya kijamii kupitia Ndugu Bandawe (PPF), kinachochelewesha ni uamuzi toka Ofisi ya Waziri Mkuu. Nashauri maamuzi yafanyike ili ginnery hiyo ianze kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili Mheshimiwa Mwijage unalifahamu, naomba uwasiliane na Mheshimiwa Mhagama ili uamuzi utolewe. Uwepo wa kiwanda hicho utachochea upatikanaji wa ajira za kudumu na muda. Ajira kwa akina mama lishe na kadhalika.

Mheshimiwa Mwijage, najua ukiamua suala hili utalimaliza haraka. Nawasilisha.