Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Mwenyekiti, uvunaji wa magadi Engaruka mradi wa kimkakati. Mheshimiwa Waziri anatambua wananchi wa Engaruka - Monduli wameridhia kuachia hekari 75,000 kwa ajili ya ujenzi a kiwanda cha magadi, lakini changamoto kubwa ni barabara. Pamoja na nia ya Serikali kutaka kujenga barabara ya Mto Mbu - Loliondo lakini ujenzi huo utachukua muda mrefu sana. Je, ni nini mkakati wa kujenga barabara hicho, ni lini kiwanda hiki kitajengwa wananchi waruhusiwe kuendeleza maeneo yao mpaka Serikali itakapokuwa tayari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiwanda cha nyama Makuyuni kimekamilika lakini tumemkosa mwekezaji wa kuendesha kiwanda hicho. Ni nini mikakati ya Wizara kutusaidia kupati mwekezaji?