Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na mimi nashukuru kupata nafasi hii lakini awali ya yote kwanza nimpongeze Mheshimiwa kaka yangu Mwijage na Naibu wake Engineer Stella Manyanya kwa kazi kubwa wanayoifanya, hongereni sana. Mungu awape nguvu ili mfikishe jahazi lenu hili, lakini nimpongeze Katibu Mkuu, Naibu wake wawili, watendaji wakubwa wa taasisi zenu, kule Sabasaba, TBS, na kadhalika shughuli tunaziona. Endeleeni kuwa na nguvu mtumikie Taifa lenu. Hongereni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nianzie kwenye kupanda bei kwa vifaa vya ujenzi. Kwenye miezi mitano iliyopita, nondo zimepanda kuanzia mwezi wa tisa mwaka jana nondo ya milimita12 ilikuwa inanunuliwa shilingi 15,000 sasa hivi unanunuliwa kwa shilingi 22,000 na nondo ya milimita 10 ilikuwa shilingi 12,000 sasa hivi ni shilingi 16,000, mabati, bundle lilikuwa shilingi 250,000 sasa hivi shilingi 300,000; saruji, ilikuwa shilingi 12,000 sasa hivi ni shilingi 17,500 kuna nini kimetokea? Wanaojenga wanauliza, kuna nini kimetokea? Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri hebu tupe majibu tuwaambie Watanzania, kuna tatizo gani kubwa limetokea ndani kwenye eneo la ujenzi kwa sababu vifaa hivi ni vya watu wa kawaida ndiyo maisha yao ya kila siku wanaojenga nyumba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili kubwa kuliko vyote, viwanda. Viwanda vingi vilibinafsishwa lakini watu waliobinafsishwa viwanda hivi wameshindwa kuviendesha.

Serikali kupitia kwa Rais Magufuli nimeshasikia mara mbili Mheshimiwa Mwijage anakwambia wanyang’anye, anakuambia na ndiyo Rais wa nchi lakini kwanini huwanyang’anyi? Hao watendaji wako kwanini hawakusaidii? Mifano hai, kuna watu wamepewa viwanda vina mashine, sasa hivi havina kitu, hivi huyu naye kumnyang’anya ni shida? Tunafanyaje kwa sababu viwanda hivi hawa watu wakinyang’anywa kuna wawekezaji watakaokuja watakuta viwanda vipo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pale Dar es Salaam kuna kiwanda kimoja kinaitwa Uzi Bora Ubungo Spinning. Kile kiwanda yule mtu ameng’oa kila kitu, watu wanakodisha mle kuweka mizigo. Ukiweka mizigo, unalipa hela yake, inaendelea. Hivi jamani, tunafanyaje? Mheshimiwa Mwijage na Mheshimiwa Stella Manyanya mnafanya makubwa, hebu waambieni watendaji walioko chini wanaowahujumu hivi navyo vinataka sense gani ili kuwanyang’anya? Mpaka iweje? Yaani ni nini kifanyike? Ukienda Masasi kule kuna viwanda pale vilikuwa vya korosho, watu wameng’oa kila kitu wanafanya maghala, wakulima wa korosho wanaenda kukodisha kwenye kiwanda chao kulipwa wakati wa msimu wa kuvuna korosho. Tufanye nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaheshimu sana hawa ninaowasema lakini naomba mje na majibu, haiwezekani, Rais amesema wanyang’anye viwanda, hamwanyang’anyi kwanini? Kwanini? Kwanini hawanyang’anyi? Kwa nini waende Mahakamani? Ukipanga nyumba ya mtu, ameweka dirisha la nondo, kesho ukiweka mbao si anakufukuza? Sasa hawa wamekuta mashine, wameondoa, wameuza, wakulima wa korosho wanaenda kupanga kwenye viwanda vyao, wanalipishwa hela! Ubungo Spinning, MSD mkienda kuangalia kwenye mahesabu alikuwa anapanga kama store, MSD ni ya Serikali, anamlipa mtu ambaye ameua kiwanda. Sasa ni muagize Wakuu wa Mikoa wapo? Wawaletee orodha ya viwanda ambavyo havifanyi kazi na watu walishavunja mikataba, kuna watu wengine wana viwanda wanachechemea kidogo kidogo lakini hawa hawachechemei, wameng’oa kila kitu wanafanya biashara yao na sisi tunawaangalia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, viongozi mliokaa hapa mnafaa na mnatosha, hebu isaidieni nchi yenu. Tuwanyang’anye vile viwanda, yabaki maghala ya nchi yetu, watakaokuja wana uwezo mpate nafasi ya kuwapa nafasi wafanye kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nihamie Mchuchuma na Liganga. Historia tunayopewa kwamba tunaweza kuchimba yale madini miaka 100 lakini tangu nimesikia utafiti tunajenga, na kadhalika ni kama miaka 12. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana nilisikia kama kuna mtu aliuliza, kwa nini kama tunaweza, tusiite watu wakaanza kuchimba tukawawekea bei wakapeleka hela Benki Kuu sisi wakati tunaendelea na utaratibu wetu? Si mmetuambia ni miaka 100, kwa nini tuendelee wakati kitu tunacho, kinatakiwa, hatuuzi, hatujengi, faida yake ni nini? Mwisho tutaondoka huku ulimwenguni hatujaona hata senti tano ya Mchuchuma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu kwenu, hebu waruhusuni wananchi wa nje, wekeni utaratibu pale, waje wachimbe wasafirishe watulipe hela, wakati ninyi mnaandaa utaratibu wenu wa kupata kiwanda. Kigugumizi cha nini? Mheshimiwa Mwijage unaweza, mimi naamini unaweza, kigugumizi kinatoka wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, watendaji wana urasimu mara mia kwa sababu sisi wanasiasa ni miaka mitano ikiisha, alikuwa Mheshimiwa Mwijage amepita, alikuwa Mheshimiwa Manyanya, amepita. Shukeni huko chini muwaambie, kama hataki kufanya si ufukuze! Si mamlaka mengine mnayo? Wimbo ni ule ule. Alikuwa Mheshimiwa Mzindakaya, ameondoka, sijui wamemweka tena nani Mwenyekiti mwingine. Wenyeviti wanabadilishana tu. Nini kinafanyika NDC kwenye hii Mchuchuma na Liganga? Mnatuficha nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tungepata umeme, tungepata pesa, lakini maamuzi hamjafanya. Nawaombeni sana mwende mfanye maamuzi ili tuone nchi hii inakwenda wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kule Mara kulikuwa na viwanda vya ginnery. Viwanda vile vilikuwa vinafanya kazi, lakini ushirika ulipokufa wakaviweka chini ya mfilisi. Ukienda pale Mgango kidogo kinachechemea, lakini mfilisi, kiwanda kinafilisika kikiwa kwenye mikono ya Serikali. Ukienda Bunda Ginnery, kinafilisika kiko pale. Ukienda kule Ushashi Ginnery, kiwanda kinafilisika kiko pale pale. Hawa wafilisi nao kwenye Hazina Mheshimiwa Mpango muungane, hawa ni akina nani? Kwa nini mfilisi anapewa mali lakini zinakuwa makopo naye yuko pale pale na ni Serikali? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapana, Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi haiko hivyo, watendaji mnaowalea watawapa madhara kwenye kuomba kura, kwa sababu wao wameajiriwa wapo. Vitu vinafia mikononi mwao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwa hiyo, maana yangu ni nini? Leo tunaenda kwenye zao la pamba, watu wanalia hapa. Ginnery zipo zilikuwa za Serikali, zinasaidia, lakini watu zimekuwa zao. Yule mfilisi ndio anakodisha kuweka pamba, anakodisha kila kitu, kesho anakwambia imeharibika. Hizi hela huwa zinaenda wapi? Kwa nini tunapata shida namna hii jamani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi wakulima pale Bukoba nilikuwa namwuliza Bukoba Town, kuna Kiwanda cha BUKOP, kile ndiyo kilikuwa kiwanda sisi tunasoma zamani kwenye KBCU. Leo kiwanda kile anacho mtu mmoja, KNCU hawana mahali pa kukoboa kahawa. Nini kilifanyika, ni shida! Ndugu zangu viwanda hivi tunavitaka sana. Tunawapongeza, mmefanya sana kazi ya kuleta viwanda, lakini vilivyokuwa vya zamani, cha zamani ni bora zaidi kuliko kipya ambacho hukioni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, turudisheni kwenye ushirika mzuri, viwanda viko chini yako Mheshimiwa Mwijage. Kama teknolojia ya zamani, waambie wang’oe walete ya kisasa, lakini viwanda viwe vyetu. Sasa tunakuwa watumwa kwenye viwanda vyetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongeze suala la Zanzibar, nataka kulisema kidogo, mnisamehe. Suala la Zanzibar hili, sipingani na Serikali yangu, lakini Mheshimiwa Turky hayupo hapa, ningemsema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini maji ya Mheshimiwa Turky yanatoka Zanzibar yanakuja Dar es Salaam yananyweka? Kwa nini sukari ile inayotoka kwenye Kiwanda cha Zanzibar haiji Bara? Kwa nini? Kwa nini haitugusi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mmefanya jukumu kubwa sana kwenye sukari, mnaweka viwanda mnaleta utaratibu, nawapongeza sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Wizara hii ya viwanda imefanya kazi kubwa sana kwenye sukari, nawapongeza sana. Kwenye sukari kwa sababu kila mwezi wa nne viwanda vinafungwa, mnatoa nafasi kidogo, watu wanaleta sukari hali inakuwa stable, lakini kwa nini kwenye sukari hapa kwenye hivi viwanda ikifika mwezi wa kuelekea Ramadhani inakuwa shida? Kwa nini? Mafuta hayapo, sukari haipo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeambiwa Mkulazi inakuja, tunawapongeza, lakini kwa nini tusiwe na bulk procurement ya sukari, Serikali ifanye kama inavyofanya kwenye NRFA? Wale watu wa vyakula, chukueni miezi ikifika tuwekeeni sukari tonnage inatosha, mafuta yanatosha, unapokaribia miezi ya Waislamu kuingia, Serikali itoe i-control. Leo hii sukari Mheshimiwa Mwijage nakuomba ukimaliza bajeti yako hamia bandarini, ili sukari iweze kushuka kule chini. Tutaingia mwezi wa Ramadhani sukari itafika shilingi 5,000 tutakuwa tunakusema wewe. Nendeni mfanye operation kama mlivyofanya ya mbolea, watu wana sukari wanafungia kwenye ma-godown sukari inazidi kupanda, kwa nini tunanyanyasika katika nchi yetu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa 90% samahani kwa kauli hii, ni watu wanaogonga passport ndio wanatutesa. Ndio!