Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia katika bajeti ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Mlalo, Tarafa ya Umba ni tambarale hivyo maji yanayotiririka kutoka milimani yanapotea bure kwenda baharini upande wa nchi jirani ya Kenya. Rai yetu ni kupata mabwawa makubwa kwa ajili ya kuanzisha skimu za umwagiliaji katika Kata za Mnazi, Lunguza na Mng‟aro. Hili ndiyo eneo pekee lenye ardhi ya kutosha katika Halmashauri ya Mlalo na Lushoto ambalo bado halijatumika.
Mheshimiwa Naibu Spika, ufugaji pia ni changamoto kwani hakuna hata josho moja. Aidha, hakuna hata mabwawa ya kunywesha mifugo ya wafugaji wa Bonde la Hifadhi ya Mkomazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Mlalo jiografia yake ni Milima ya Usambara na kuwa kikwazo kwa shughuli za uvuvi kwa kuwa hakuna mito na maziwa. Tunaomba Wizara ituweke katika mpango wa kutupatia mabwawa ya samaki ili wananchi wangu waweze kupata bidhaa hii katika ubora na kuondokana na tatizo la kuwa na upungufu wa madini ya chuma.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna tatizo sugu la ufungaji wa mazao kwa mtindo wa lumbesa na kuwanyonya kwa kiasi kikubwa wakulima ambao wengi wao ni wanawake na wanalima kilimo hai ili waweze kupata tija ya mazao yao.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili tuendeleee tunahitaji mambo manne muhimu nayo ni ardhi, watu, siasa safi (good policy) na uongozi bora. Mheshimiwa Waziri hakikisha kupitia halmashauri nchini tunaweka utaratibu wa kuweka Reserve Land Bank ili wakati tunapopata wawekezaji wa kilimo tuwaelekeze huko.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia tuwajengee uwezo watu wetu hasa wafugaji ili kupata namna bora ya kuwashawishi kupunguza idadi ya mifugo na kupata tija wawapo na mifugo michache. Vile vile badilisha sera ambazo siyo rafiki kwa Wizara yako ikizingatiwa Wizara hii ndiyo mhimili wa uchumi wa Taifa, pia ndiyo chachu ya kuelekea Tanzania ya viwanda.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama mnataka mali mtaipata shambani.