Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Ahmed Juma Ngwali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ziwani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. AHMED JUMA NGWALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nataka nianze kidogo na ufanyaji biashara baina ya Tanzania Bara na Zanzibar. Wakati anahitimisha Waziri wa Muungano na Mazingira, Mheshimiwa January Makamba alisema kwamba kutokana na kero za ufanyaji wa biashara kuwa nyingi, wanadhamira/wanakusudio kuiunganisha Zanzibar katika mfumo wa TANSIS ili kurasimisha kodi za pamoja baina ya Zanzibar na Tanzania Bara ili kuondoa hilo jambo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napingana sana na jambo hili kwa sababu unaporasimisha kodi za pamoja, Zanzibar watakuwa katika wakati mgumu sana, itawalazimu washushe kodi zao za ndani na mimi nistaajabu sana Serikali ya Muungano kwa nini watu wanachukua hizi baadhi ya kelele wanataka kuleta jambo ambalo litaongeza tatizo la mzozo wa Muungano kuliko ilivyo sasa. Kwa hiyo, niiombe tu Serikali kwa sababu dakika sina, hili jambo la kuiunganisha Zanzibar katika Mfumo wa TANSIS wasilifikirie kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, Mheshimiwa Mwijage ni kwa nini Kenya, Tanzania na Zanzibar na nchi nyingine tu zimepiga marufuku kabisa utengenezaji na uingizaji wa mifuko ya plastiki katika nchi. Tuna viwanda 41 tu ambavyo vinatengeneza mifuko ya plastiki ambapo viwanda hivyo vinazalisha asilimia tano tu, asilimia 95 inakuwa imported kutoka nje. Sasa kuna tatizo gani? Nyuma ya mfuko wa plastiki kuna nani ambaye anashinikiza viwanda hivi viendelee na tuendelee kuharibu mazingira jambo ambalo litatusababishia madhara makubwa kama Taifa, nini nyuma yake kuna kitu gani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa haraka haraka niende katika suala zima la viwanda na umeme. Tumebishana na tumezungumza sana kuhusu umeme, wengine wanazungumzia kuhusu Stiegler’s Gorge lakini na wengine wanazungumzia kuhusu umeme wa gesi lakini energy mix ndiyo inayotumika duniani kote, hatuwezi kuwa na umeme wa kutegemea mfumo mmoja tu wa umeme. Lazima tuwe na umeme, huku upatikane na huku upatikane. Lengo letu sote tunajenga nyumba moja, lengo letu ni kupata umeme ambao utafika megawati 5,000 na zaidi. Hizo ndiyo dhamira ya Serikali na mimi nakubaliana nao kwenye energy mix kwenye jambo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu Mheshimiwa Mwijage na Ofisi ya Waziri Mkuu, ninyi ndiyo mnaratibu mradi wa Bagamoyo ambao mkatutamanisha, mkatumbia eneo hili ni la SEZ tutapata kuweka, tutajenga bandari kubwa ambayo itakuwa meli za kizazi cha nne zitafunga. Wenzetu Kenya tayari meli zinafunga. Meli ya mita 300 karibuni tu ilifunga, sasa sisi meli meli kubwa ambayo MV Lienna ambayo ndiyo ina mita 420 tulidhani itakuja kufunga kabla Kenya haijafunga, lakini mpaka leo mradi huu unasuasua. Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo inaratibu kwa sababu jambo hili linaratibiwa na watu wengi, inakuwa shida hamtuelezi, hakuna maelezo ya kutosha yanayoonesha kwamba jambo hili litamalizika kwa muda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la nne kwa haraka haraka; Mheshimiwa Mwijage, Serikali iseme tu kama imeshindwa kuzuia bidhaa bandia zinazoingia nchini. Tumeanzisha mfumo wa PVOC ambao ni free shipment kule kuzuia lakini mpaka leo bidhaa fake zinaingia. Tumeanzisha hiyo halafu tukasema tutafanya Direct Inspection (DI) hapa bandarini lakini bado bidhaa fake zinaingia. Lakini polisi ambao unasema, nilikuwa nasoma kitabu chako mnataka kutumia mpaka Interpol kuzuia bidhaa fake. Polisi hao wenyewe ndiyo wanaoshiriki katika mambo hayo ya kuingiza hizo bidhaa feki, hiyo Interpol gani mnayotaka kutumia? Mheshimiwa Mwijage hilo rekebisheni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo la tano Mheshimiwa Mwijage suala la gypsum. Gypsum paper zinaingia kwa asilimia 25, gypsum board zinaingia za asilimia 45. Sorry ni asilimia 25 kwa 25. Kwa hiyo, zikiingia 25, 25 ushindani ndani ya viwanda vya ndani haiwezekani kwa sababu tuna uwezo, tuna viwanda vinne vya gypsum kama sikosei, lakini vinazalisha gypsum board milioni 25 kwa mwaka. Demand ya Tanzania ni milioni 10 au 12, sasa tunalinda viwanda au tunabomoa viwanda? Kwa hiyo na hilo pia lirekebisheni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme jambo la mwisho, sio la mwisho kama muda utakuwepo lakini kwa mfano teknolojia, tuna CAMARTEC, tuna TEGRO na kadhalika zinatumia teknolojia ya kizamani wakati mwendo wa teknolojia sasa hivi umebadilika.