Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niungane na Watanzania wapenda mema, watakia mema Taifa hili, kumpongeza Waziri wangu kivuli Mheshimiwa Joseph Mbilinyi kwa kumaliza kifungo chake, lakini tunamwambia kwamba alipaswa kupitia hayo ili kuleta ukombozi katika Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sote tunafahamu Mwalimu Nyerere aliamua kuufanya Mkoa wa Morogoro kuwa ni wa viwanda. Tukiacha Mkoa wa Dar es Salaam mkoa wa pili kuwa na viwanda vingi ilikuwa ni Mkoa wa Morogoro. Na kuanzia miaka ya 1960, 1970 kuendelea mpaka ya 1980 kwa Mkoa wa Morogoro huwezi kumkuta house girl kutoka Morogoro anaenda kufanya kazi, huwezi kuwakuta vijana wamekaa vijiweni, huwezi kuwakuta hata wazee wanakunywa kahawa vijiweni kwa kuwa watu wote walikuwa na fursa ya kuingia kwenye viwanda, kufanya kazi kwenye viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Serikali lengo la kubinafsisha viwanda ni kuongeza efficiency, lakini cha kushangaza, kwa makusudi mazima watu wale waliihakikisha Serikali kwamba watavichukua viwanda, wataviendeleza na kuhakikisha ajira inaendelea kuongezeka na kuongeza. Sasa badala ya ku-expand viwanda, kuongeza ajira watu wamevitumia viwanda kama collateral kwenye kukopa na kufanya biashara zao zingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maana hiyo viwanda vya Morogoro vimekufa kwenye mikono ya watu, watu wamekosa ajira na tunategemea na Waziri wakati anahitimisha atuambie, Serikali imechukua hatua gani kwa watu hao ambao wameua viwanda kwa makusudi kabisa. Serikali imechukua hatua gani kwa watu hao ambao wamewanyima Watanzania ajira? (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. DEVOTHA MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipokea taarifa na ninaamini Waziri amemsikia vizuri Mheshimiwa Kuchauka alichokisema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna tegemea Waziri na hitimisha atuambia hivi Morogoro tunahitaji viwanda vingine vipya, kama anavyosema ama tunahitaji kwanza tufufue vilivyoko? Kwa sababu rasilimali ya viwanda tayari tunavyo. Lakini sasa hivi vimekaa tu kwa hiyo tunataka kuona mpango wa Serikali katika kuhakikisha wanafufua viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukizungumza kuhusu viwanda ambavyo vilikuwa vikitengeneza malighafi, nimemsikia Waziri pale wakati anawasilisha, katuonesha na viatu ambavyo vimetengenezwa, hivi Mheshimiwa Waziri nikuulize, ngozi zinaharibikia Morogoro hatuwezi kuzitumia unatuonesha viatu, tunashindwa ku-export ngozi pale Morogoro, nilikuwa nauliza lengo lilikuwa ni nini kama kweli tuna ngozi ambazo tunashindwa kuzitumia, unatuonesha sample ya viatu vichache. Ungetupa mikakati ni nini Serikali imejipanga kufanya kuhakikisha hata Viwanda vya Ngozi vilivyopo Morogoro ambavyo vimesheheni ngozi ambazo wanashindwa kuziuza mpango wako ni nini vitengenezwe viatu kama ulivyotuonesha? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kiwanda cha Mbigiri, tumesikia Serikali inataka kuanzisha Kiwanda cha Sukari. Lakini fidia kwa wananchi waliokuwa katika eneo hilo ni kilio mpaka sasa hivi. Kwa kweli watu ambao waliendeleza maeneo haya ambayo yaliachwa na Serikali miaka mingi wanakuja kuambulia patupu, halafu mnawaambia eti mtawafundisha kuwa ni out growers ambao hawana maeneo, hii si sahihi kabisa. Na nishukuru nilimuona Mheshimiwa Waziri anajaribu hata kulima kule anawaonesha jinsi ya kulima, lakini watalima wapi Mheshimiwa Jenista? Maeneo mengi yamechukuliwa, hawana pa kulima mnategemea out growers watatoka wapi Mbigiri? Kwa hiyo, Serikali inapojipanga ione namna gani yakuwasaidia na wananchi ambao wanazunguka maeneo ya viwanda ambavyo mnataka kufanya kazi ili wale watu waweze ku-support viwanda hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumesikia Serikali ikisema ina mpango wa kuweka viwanda 100 kwa kila Mkoa. Hivi najiuliza, hivi viwanda tunavyovizungumzia ni vipi? Ni viwanda plant, tunazungumzia viwanda vidogo au tunazungumzia viwanda vya aina gani? Kwa sababu hivi sasa kuna viwanda vikubwa Dar es Saalam ili kifanye production ni lazima umeme ukatike Dar es Salaam nzima. Sasa tunataka kupeleka viwanda vya namna gani kama hatua umeme wa uhakika, hatua barabara zinazoeleweka, hatuna maji ya kutosha, hivi ni viwanda gani mia tunapeleka katika Mikoa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri anaelewa kabisa kwamba kuna baadhi ya maeneo wawekezaji wanaombwa leo mzalishe usiku ili Watanzania wengine wapate umeme. Kwa sababu wakizalisha umeme wote unaotumika mkubwa unalazimika kuingia kwenye kiwanda. Kwa hiyo, mimi nafikiria kabla ya kuja na idea ya viwanda hakikisheni tuna umeme wa kutosheleza, hakikisheni zipo barabara za kutosheleza zitakazokwenda vijijini kuchukua mazao. Lakini zaidi barabara pamoja na kuhakisha maji yanatosha katika hivi viwanda. Tunaelewa hivi viwanda vinahitaji maji ya kutosha. Kwa hiyo, idea ya kusema tu viwanda, viwanda tunaona hii ni kama tu kuwadanganya Watanzania Serikali hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu huwezi kwenda kwenye viwanda huna mipango sahihi ambayo tukitizama tunaona kweli tunaelekea kwenye viwanda. Unless utuambie twende kwenye viwanda vya vyerehani, vyerehani havihitaji maji, vingine hata havihitaji umeme tutakuelewa. Lakini plant tunazozitaka sisi ziende sambamba na miundombinu ya kuwezesha viwanda hivi viendelee kutoa ajira kwa Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kusema hayo nakushukuru.