Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ANATROPIA L. THEONEST, Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, kuna msemo mmoja ni maarufu sana kutoka kwa muhenga mmoja anaitwa Napoleon aliwahi kusema; let China sleep for when the dragon wakes she will shake the world. Alisema Uchina wamesinzia, lakini siku ikiamka dunia itaona. Nataka hilo swali niimuulize ndugu yangu, Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara anaiambia nini Tanzania? Wakati na Napoleon akiiona China na kuiambia dunia msione dunia imesinzia ikiaamka itakuwa balaa yeye anatuambia nini? Anatuambia nini wakati tumekuwa tunaongelea changamoto kadha wa kadha za viwanda zikiwa zinajirudia, wakati tunarudia yale yale na kila bajeti inayokuja tuna address yale yale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nitalia na kitu kidogo sana EPZA ninafahamu sisi kama Tanzania tuna copy uchumi wa viwanda kwa lengo nzuri la kwenda kuwa Serikali ya uchumi wa kati au nchi ya uchumi wa kati kwa vision yetu ya 2025 tukiangalia Tiger Nations, tukiangalia Taiwan, Singapore na South Korea, walifanya nini? Wameingia kwenye viwanda ndio, na sisi tunaingia kwenye system viwanda tena kwa wazo la ku-fast track which is good. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tuna - fast truck kuingia kwenye viwanda je tunaangalia wao walifanya nini walijikwaa wapi au kipi walifanya vizuri zaidi ili na sisi tukichukie. Wali-focus kwenye export na mimi ninafurashi kwamba nchi yangu kupitia kwa Waziri Mwijange mnawaza au tunawaza ku-export, lakini ni kwa kiwango gani tume- capitilize kwenye ku-export. Tumekuja na kitu, nimesema nitasemea kitu kinaitwa EPZA, tumefanya nini vya kutosha kuandaa maeneo ya uwekezaji, swali kila wiki swali kila mwezi tunaongelea maeneo ambayo bado madeni ya EPZA lakini pia fedha inayotengwa haitoshi. Nimesoma Fungu 44 katika sera mmeonesha kwamba mmetenga bilioni 1,200,000,000 lakini kwenye kuandaa miundombinu na vitu vingine kadha wa kadha mmeandaa bilioni moja. Nataka mniambie hiyo fedha kidogo itaweza kufanya nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, EPZA ndio msingi mzima wa biashara, msingi mzima wa biashara kama tunateka kwenda 2025 kama nchi ya uchumi wa kati, ni lazima tu-export zaidi. We have to export more, ndio new Tiger’s country walichokifanya. Tuna-export nini? Hilo ni swali la pili, maana nchi hizo za Singapore nchi kama South Korea walikuwa very specific kwamba tunataka tu-capitalize katika moja, mbili, tatu sasa sisi tunataka tu-capitalize katika nini. Tunaweza tukawa na viwanda vingi nchini lakini tunataka dunia itufahamu katika nini? Ukiisema Kenya leo, watakwambia katika Afrika, Kenya ni mzalishaji mzuri wa coffee na tea. Lakini je, Tanzania tuko katika nini? Ni lazima tu-capitalize tunataka kufanya nini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninarudi tena kwenye EPZA, hizo bilioni moja mlizotenga zinatosha kutengeneza miundombinu? Kwenye hotuba yako umeonesha hapa, kwamba tunataka tuweze kutengeneza ukuta wa EPZA ya Benjamini Mkapa umedondoka; tunataka tuweke miundombinu ya maji ya EPZA ya Mkapa kwa sababu haipo. Hivyo ni vitu ambavyo vinaleta ukakasi, ni vitu ambavyo haviwezi kuvutia zaidi wawekezaji. Lakini pia kama haitoshi nimeangalia kwenye the easy of doing business. Watu wanavyokuja kuwekeza fedha zao kutoka duniani kitu cha kwanza wata-google wewe ndio unasema hapo Tanzania, Tanzania ikoje, bado tuna-rank 137 hatujafanya vizuri. Kama tunataka ku-fast track kama tunataka tuwe uchumi wa kati by 2025 hatuko mbali na 2025 guys kama tunadhani tunakaribia huko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika report ya CAG ameeleza wawekezaji, niseme sampling aliyoifanya ya viwanda kumi na moja au ya wawekezaji 11 kati ya 57 ambao wamewekeza kwenye EPZA waliahidi wangekuwa na mtaji wa bilioni 131.5 lakini kwa mwaka uliopita wanaonekana wamewekeza only 33% ambayo ni shilingi bilioni 43. Wametudanganya wapi, tumewapokeaje kama wanaleta makaratasi na sio fedha au pengine walikuja na fedha zao wamekutana na vikwazo kadha wa kadha ambavyo tunazidi kuviongelea hapa. Vikwazo kama gharama kubwa ya uzalishaji, gharama ambazo mnatusabibishia leo mnatuambia tunalazimika kununua sukari shilingi 110,000 badala ya shilingi 65,000 kwa lengo la kulinda Viwanda vya ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hatuwezi ku-compete kama hatutashuka chini tukapunguza gharama za uzalishaji tukazalisha bidhaa nzuri tuka-export nje hicho ndio walichokifanya New Tigers Contries, lakini ningeweza kutoa ushauri mdogo wenzangu wamesema, tunaweza kuamua kwamba tunataka ku-focus katika kitu gani, umeonesha kwenye kitabu chako hata hivyo uchumi wa viwanda haujachangia kwa kiwango kikubwa sana. Ukurasa wa 185 haujachangia sana katika pato la Taifa. Tunaona asilimia saba, 6.9% mpaka 5.5% consecutive ambayo ni ya 2017. Ni changamoto kubwa sana tuna hicho kiwango kidogo ambacho kinachangia katika uchumi wa Taifa kama tungeweza kuwekeza katika sekta zinazowa-accommodate watu wengi tungekuwa tunaona mabadiliko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tungeweza kuona mabadiliko tena kwa macho, umesema kuna uzalishaji wa pamba nchini na viwanda 11 ambavyo ni processing lakini havifanyi vizuri. Ukurasa wa 22. Ukasema ni asilimia 30 tu ya pamba inayozalishwa nchini inatumika instead 70 percent inakuwa exported tukiamua kuji-reduce tu kutafuta wawekezaji katika viwanda vya nguo ambao ndio kitawa- accommodate watu wengi ambacho ndio kilimo actually ndio walichokifanya nchi ambazo tuna-copy mfano. Ndio walichokifanya hata South Korea tunayoisema. Walianza kuwa na viwanda vya kawaida baadae waka- revolutionaries agriculture yao, sisi bado tuna nafasi nzuri tuna eneo kubwa kwa maana ya ardhi, tuna wakulima, tuna watu wenye hali, tungeweza kuwa tumewafikia watu wengi, tungeweza kubadilisha Tanzania, tungeweza sasa kuingia kwenye a mid ecomonic countries kwa wepesi kushinda nguvu kubwa ambayo tutaenda kuitumia kwa viwanda vya propaganda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kikubwa ambacho ninaomba nisisitize hapa ni tunafangamanisha vipi elimu yetu na uchumi wa viwanda? Katika ku-rank 137 duniani ni wanaangalia na skilis na watu, wale watu wanaoleta viwanda vyao pia wanaangalia hiyo labour force ikoje? Sasa labour force ya vyuo ambao so far wako theoretical na siyo practical itazidi kutu-pull down. Ni lazima tufungamanishe uchumi wetu na viwanda na elimu yetu.