Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi hii walau na mimi ya kuweza kutoa mchango wangu katika Wizara hii ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kutoa pongezi nyingi sana kwa Waziri huyu wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, pamoja timu nzima katika Wizara ya Viwanda, Katibu Mkuu, Watendaji wote FCC,TBS,TRA na wengine wote huko chini ninawapongeza sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nianze tu yaani kwa kusema maneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba sana Wizara hii ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji ukianza Waziri pamoja na watendaji wako ichukuliwe kwa umuhimu wa kipekee, mtoke nje. Jana iligusiwa kidogo na Mheshimiwa Spika wetu, na mimi kitu ambacho nimekuwa nikikifikiria sana Wizara hii kuna baadhi ya watendaji kule chini ambao vitu vingi sana wanavifanyia mezani, hawajui on the ground, kwenye hali halisi kule mambo jinsi yalivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mimi ninaomba na biashara ni ushindani na baishara msingi mkubwa wa biashara ni connection. Kwa hiyo, Waziri wetu pamoja na watendaji wote, Wakurugenzi yaani mimi nitafurahi sana endapo kama nitaanza kusikia Mkurugenzi wa FCC,
Mkurugenzi wa TBS wamekwenda huku na huku, wasikae ofisini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hizi kazi zao si kazi za kusubiri tu kwamba mtu amefanya makosa ndipo aje huku kuja kmshughulia, inatakiwa na wao waende on the ground, waende kule kujifunza. Ninasema hivyo kwa sababu gani, kuna nchi jirani zawenzetu ambazo tunapakananazo, haiwezwekani sisi tukawa na urataibu mwingine nchi za wenzetu zikawa na utaratibu mwingine, Serikali inakosa mapato. Mfanyabiashara yoyote duniani hata kama mtu mkiwa mama ntilie nia yake anataka apate faida na sio tu faida akipa upenyo wa kuongeza faida kubwa yeye kwake ndiyo anaona ndiyo mafanikio ya baishara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapokaa kuzungumzia uchumi, uchumi ni biashara, hauwezi kutenganisha uchumi na baishara. Sasa basi nikupe tu mfano kwa mfano sisi kama Watanzania kwa wezetu ambao ni wafanyabiashara kuna bidhaa ambazo kwa nchi za wenzetu kule kwao ni zero tariff. Lakini hapa kwetu tumeziwekea tariff, lazima na sisi tuweze kuangalia kwa nini wale wenzetu kule wamefanya hivyo ili nasi huku tuweze ku-react haraka. Kwa sababu kwa mfanyabiashara ambaye anajua biashara ataona kwamba nikiingiza Tanzania nitapata hasara, kwa hiyo atakachokifanya ataenda kukimbilie kuingiza huko jirani kwenye nchi za wezetu jirani ambako kule zinaingia kwa bei ya chini alafu baadae zitakuja kuigia huku Tanzania. Kwa hiyo mimi nilikuwa naomba sana Serikali iweze kuangalia kuhusu hili suala. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine ninapongeza sana hii Wizara na ninampongeza sana Mheshimwa Rais. Hata leo hapa tunavyozungumza ni miaka takribani miaka miwili na wala si miaka mingi sana, lakini wamefanya kazi kubwa sana wanajitahidi sana. Mheshimiwa Waziri usijali baadhi ya madongo unayopigwa pamoja na wenzako, madongo hayo unayopigwa mimi huwa wakati huwa najiuliza natamani na huwa mara nyingi sana nasema kwamba natamani yaani huwa wakati mwingine nasema kwamba ndiyo maana sasa nailewa baadhi ya nchi duniani viongozi waliopita kwenye nafasi mbalimbali kama Mawaziri, Makatibu Wakuu na kadhalika kuna baadhi ya nchi huku Mawaziri walikuwa wanapigwa mawe na wanafanyiwa hivi kwa sababu ya mambo waliyofanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hi inapata matatizo mengi sana na Serikali hii imekuwa ikipata mataizo mengi sana kwa sababu ya system ambayo ilikuwa imeoza iliyopita. Nitoe mfano, utaratibu wa TRA wa zamani maana na mimi si mfanyabiashara mkubwa, lakini walao nakaakaa karibu karibu na wafanyabiashara, utaratibu wa TRA wa zamani ilikuwa ni kwamba mtu lazima utoe rushwa ili mambo yaende, ilikuwa ni kwamba lazima utoe rushwa huku na huku ndipo mambo yako yaende. Sasa basi mfanyabiashara/mtu yoyote ambaye anataka biashara yake na apate faida alikuwa anaona kwamba huo ndiyo utaratibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kwa sababu huo ndio utaratibu wafanyabiashara walikuwa wanalazimika kufanya vitu ambavyo vilikuwa wakati mwingine ni kinyume na maadaili.

Sasa ninachoiomba Serikali kwa sasa hivi tujaribu kukaa chini kuangalia, hawa wafanyabiashara si watu wa mataifa mengine, baadhi yao ni Watanzania wenzetu. Hata kama mtu akiwa pengine labda ana rangi tofauti lakini bado pia ni Mtanzania mwenzetu, wapo hapa Tanzania wanataka kuendelea kufanya biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tusiendelee na yale mambo ya kukaa kuangalia yaani wao ni kwamba kama sheria imekaa, kama kanuni na taratibu tumekaa, tumesema kwamba hawa watu walifanya mambo mabaya tukae nao, najua kwamba Serikali kamba imekaa nao imewasikiliza, imeweza kuangalia kwamba wewe ulikwepa kodi mwaka fulani, lakini baada ya hapo tujiulize huyu mtu anaendelea na biashara au haendelei? Kama anaendelea Serikali iweze kumwangalia kwa macho mawili na kwa ukaribu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile isichukuliwe sasa kwamba mfanyabiashara kwa sababu miaka ile ya nyuma alikuwa labda pengine inasemekana kwamba aliwahi kukutwa tuhuma za kufanya jambo fulani, kwa sasa hivi anaendelea kuzibiwa kwa asilimia 100. Tusiendelee kufanya namna hivyo sisi tunachotaka hizi kodi zitusaidie kwenye nchi yetu nchi yetu ili nchi ipate pesa. Hawa wafanyabiashara hawajakimbia nchi, wapo wengine ambao si wazalendo wameamua kukimbia nchi, lakini hawa wafanyabiashara kama walikuwa na madeni yao kaeni nao huko mkubaliane nao kwamba watalipaje hizo pesa walipe Serikali ipate pesa. Lakini tusiendelee kusema kwamba wafanyabiashara fulani, kwa mfano labda Lucy Mayenga huyu inasemekana kwamba alikuwa anafanya jambo fulani basi ndo anakuwa ameharibika kiasi kwamba mpaka sasa hivi hata akiingiza mizigo yake anapata usumbufu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiendelea kufanya namna hiyo biashara za watu zitakufa, kodi ambazo sisi kama Serikali tumekuwa tukifikiria kuendelea kuzipata hatutaendelea kuzipa kama inavyotakiwa. Pamoja na hayo ninataka kwamba Serikali iendelee kufanya utaratibu kama inavyotakiwa. Kinachotokea sasa hivi kwa hilo ambalo linaendelea ni nini, kwa mfano mimi kama mfanyabiashara nina kampuni yangu inaitwa X inaonekana kwamba labda inasakwama sana kutokana na mambo ambayo labda pengine nilifanya huko nyuma, labda pengine tumekaa chini tumekubaliana kwamba jamani nilikuwa nadaiwa nitalipa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtu anaamua sasa, kwa mfano Mheshimiwa Waziri nikupe mfano mmoja, mfano tu mdogo TIN Number mpaka mwendesha boda boda anayo. Mimi nikileta leo hii makontena kumi kwa ajili kampuni yangu ninyi kama Serikali mtu akija akanikanidiria makadirio ya juu natafuta watu wa bodaboda kumi kila mtu pale na TIN Number yake anaingia ule mzigo kama vile kwamba ule mzigo ni wa kwake. Kwa maana hiyo sasa Serikali itakosa income tax na itakosa VAT return. Kwa hiyo, lazima tukae tuangalie, biashara ni vitu lazima wakati wewe unafikiria (a) uangalie (b), (c) na (d). (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niongezee tu hapo; kama sisi tunafahamu Serikalini kwamba asilimia 30 ya pato la Taifa linatokana na wafanyabiashara wakati na wadogo lazima tuangalie kwamba tunawezaje kuweka mazingira mazuri. Mheshimiwa Rais amekaa na wafanyabiashara, uamuzi wa Mheshimiwa Rais kukaa na wafanyabiashara si uamuzi mdogo. Ameamua kukaa na wafanyabiashara kwa sababu anachotaka haya mambo na malalamiko anataka kwamba watu wakae tuanze upya, kazi zianze kufanyika upya na mabo yakae yawe sawasawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho kabla sijagongewa kengele ninachoomba kusema, ninaomba kusema ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni Mwenyekiti wa Kamati ya Viwanda na Biashara, ninaomba na sisi wanasiasa kwa ujumla na hasa sisi Wabunge tusiwe madalali wa wafanyabiashara. Sisi kwenye Kamati yetu tulikuwa na Mheshimiwa Munde Tambwe, tumekaa kuna baadhi ya vitu tulikuwa tumekaa tukasema hivi hatuvikubali. Kuna mtu mmoja ambaye alikuwa ni mfanyabiashara anadiriki mpaka kiwango cha kuongea lugha mbaya na bahati yake ni kwamba sisi hatukuwepo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niliwahi kusema kwamba kwenye mambo ya msingi, mambo ya uchumi mambo ya kulitakia mema Taifa letu lazima sisi wana siasa tuanze kwanza, hata kama ukiongea uongee yale ambayo unaona kabisa kwamba haya ni mambo ya ukweli ili kuweza kulisaidia Taifa letu. Tusikae tu kwa sababu sisi tuna interest, una interest zako binafsi huko pembeni unataka watu wote wakukubalie waseme ndiyo, for what? Ni kitu ambacho hakiwezekani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mwisho kabisa kabla sijagongewa kengele, shilingi bilioni kumi na tatu za kulipa fidia Liganga na Mchuchuma Mheshimiwa Waziri nilikuwa naomba hizi pesa ni nyingi sana. Kabla ya kulipa hizi pesa bajeti yako ikishapita nenda kajiridhidhishe uangalie pesa hizi.