Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Mariamu Ditopile Mzuzuri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MARIAM D. MZUZURI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi kuweza kutoa mchango wangu kwenye Wizara hii ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jambo moja naomba nilitolee ufafanuzi. Serikali iliyokuwepo madarakani ni Serikali ya Chama cha Mapinduzi; Serikali ya Awamu ya Tano ya Chama cha Mapinduzi na inatekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015/2020. Sasa leo hii unatofautishaje Serikali ya Chama cha Mapinduzi na Serikali ya Chama cha Mapinduzi. Awamu ya kwanza ilikuwa ni ya CCM, ya pili ya CCM, ya tatu ya CCM, ya nne ya CCM na ya tano ya CCM. Leo hii Mheshimiwa Rais Magufuli akizindua kiwanda ambacho jiwe la msingi liliwekwa na Kikwete hapo kuna tatizo gani? Maana watu wanaleta hoja ambazo hazina mashiko. Tumepewa nafasi hii kutoa michango naomba tutoe michango ambayo inaleta tija. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano mdogo tu mimi Mzaramo nitatoa mfano, leo hii kaka yangu Kubenea ameenda kuoa baada ya harusi akitembea na mke wake watu watamsifu, Kubenea una mke mzuri, alimlea yeye? Ni kwa nini wasisifie wazazi waliomlea yule mke. Nimetolea
mfano, utapewa sifa wewe mume wa yule mke ingawa hujamzaa wala hujamlea wewe. Kwa hiyo, mafanikio ambayo leo hii tunajivunia ya awamu ya tano yanatokana na misingi mizuri ya Chama cha Mapinduzi na Serikali zake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais alivyokuwa anaomba ridhaa ya kuongoza nchi hii wimbo wake mkubwa ulikuwa kwamba tutajenga Tanzania yenye viwanda na ninampongeza. Mheshimiwa Rais ameanza kuweka mikakati ya kitaifa ambayo itatupeleka kwenye uchumi wa viwanda. Uwekezaji kwenye reli ulio kwenye kiwango cha standard gauge, kinaenda kuwekeza kwenye uchumi wa viwanda. Ununuzi wa ndege ambao tunafufua Shirika letu la ATCL leo hii lazima tutambue tunasafirisha minofu ya sangara kwenda nje ya nchi, tunasafirisha maua, tunasafirisha mboga mboga. Leo tumeanza kununua ndege za abiria ndogo mpaka kubwa, najua huko mbele tutaenda kununua ndege za kusafirisha mizigo. Kwa hiyo, zile bidhaa zetu tutazisafirisha kwa shirika letu, tuta-enjoy economies of scale. Kwa hiyo, lazima tutambue kwamba uwekezaji huu kwamba Mheshimiwa Rais anasimamia kauli yake na kwa level yake ya juu kabisa ameonesha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kwenye uwekezaji wa Stiegler’s Gorge kwenda kuzalisha umeme yote hii tunaona kwamba tunaenda kuelekea kwenye uchumi wa viwanda. Waliokuwepo chini ya Mheshimiwa Rais, Waheshimiwa Mawaziri hususani Waziri Mwijage, kama uthubutu wa Mheshimiwa Rais kuwekeza kwenye haya mambo je, wewe unaendana naye? Kila saa anasimama Mheshimiwa Rais kuwaambia wasaidizi wake hivi kweli mnaelewa mimi ninayoyahitaji? Je, mnasoma mimi nini ninachokitaka? Tunakuomba Mheshimiwa Mwijage lazima ujiulize mtu akikusifia makofi matatu hayazidi. Kwa hiyo, je, unaendana na ajenda? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba, mimi nina neno moja kwa Mheshimiwa Waziri naomba uwe serious kwenye hii ajenda ya viwanda na uwekezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la tatu tunaenda kujenga viwanda na viwanda tayari vipo vya ndani tunavilindaje? Maana kuanzisha kiwanda ni jambo moja, lakini kuvifanya viwanda hivi viwe endelevu na vizidi kukua lazima tuweke ajenda muhimu je, Mheshimiwa Waziri naomba ukiwa unakuja kujibu hoja utuambie una mipango mikakati gani gani ya kulinda hivi viwanda ambavyo tunavianzisha? Unaweza ukaanzisha viwanda vikatoa bidhaa visinunulike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii tunawaambia wananchi wetu tuwe wazalendo tununue bidhaa za ndani, lakini unaweze ukakuta nguo kutoka China ina bei nafuu kuliko nguo iliyotengenezwa Mwatex na haya matatizo tunasababisha wenyewe, viwanda vya ndani vinaonewa, urasimu ni mwingi, umangimeza umejaa, utitiri wa kodi na usumbufu ambao hauna sababu. Mwenye kiwanda atafuatwa Halmashauri, atafuatwa na Mbunge, Diwani, OSHA na Wizara, yaani imekuwa ni usumbufu. Tunawaambia wawekeze hela, tunawapa pressure katika kurudisha mitaji yao na kuweza kujiendeleza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitatoa mfano mdogo, leo hii mtu akileta nyuzi ama nguo kutoka nje ya nchi, ataleta estimates za uongo atawekewa kodi ndogo, lakini huyu mwenye kiwanda ndani atakuwa charged kodi nyingi, hatimaye cost of production inakuwa kubwa anashindwa kufikia break even, anafeli. Kwa hiyo, lazima tuangalie na tuwe na mikakati. Naomba na nasisitiza ukiwa unajibu hoja unijibu kwamba una mikakati gani katika kulinda hivi viwanda na uwekezaji wa ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu chochote lazima kiwe na washika dau. Waheshimiwa Mawaziri wote kwa ujumla hasa Waziri wa Viwanda, jamani msiwaogope wafanyabiashara na wawekezaji, hii inaenda kwenu Waheshimiwa Mawaziri na watendaji, mfanyabiashara ataomba appointment na kuonana na Waziri au mtendaji mtamkwepa, mnamkwepa nini. Yule ndiye mdau wako, kaa naye ujue changamoto zake na yeye umueleze mambo na mikakati ya Serikali. Utapigiwa simu na mwekezaji aah naogopa, hutaki kumuona wa nini? Utapata wapi information za kukusaidia? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama mtu mla rushwa atakuwa mla rushwa tu, rushwa zina aina nyingi sana kupatikana, kwa hiyo, tusiwekewe hawa watu. Pia nikupongeze MheshimiwaMwijage maana naona jana ulialika wadau wako wamiliki wa viwanda akiwemo Mzee wangu Kilua mmiliki wa Kilua Group. Kwa hiyo, hilo nalo nikupongeze, lakini wengine wote tusiwaogope hawa ni wenzetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanasema when government walks, business community runs. Kwa hiyo hawa ni wadau wetu tusiwakwepe, tukae nao tujue changamoto tuweze kusaidiana kupeleka gurudumu la maendeleo mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala naomba niliweke vizuri na na-declare interest kwamba mimi ni mkulima na ni mchuuzi wa mazao. Kwa hiyo, nikiongelea natafuta soko la ufuta nafuatilia kwenye soko la dunia na vilevile nchi za wenzetu hali yao ya kuvuna, maana lazima tuelewe si Tanzania peke yake duniani ndiyo inayolima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa taarifa tu mtambue kwa mujibu wa FAO, India ndiyo nchi ya kwanza inayolima mbaazi duniani, lakini India ndio nchi ya kwanza ambayo pia inanunua mbaazi duniani. Yote ni kwa sababu India ndiye mtumiaji wa kwanza wa mbaazi, tofauti na chakula India anakamua mbaazi mafuta. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilichotokea msimu wa mwaka 2017/2018 kuhusu mbaazi maana shutuma nyingi zinakwenda kwa Serikali, penye kushauri tushauri ukweli, penye kukosoa tukosoe ukweli na kwenye kusifia tusifie ukweli. I am talking because I know. Mimi nilikuwa nafuatilia suala la mbaazi, kilichotokea msimu uliopita India ili-over produce mbaazi. (Makofi)

Mimi nilikuwepo kule na nikaenda Lower House Bungeni kwao na siku hiyo nilikuta mjadala Wabunge wa Upinzani wamewachachamalia Serikali wakiwaambia najua mmeenda nchi za Afrika ikiwemo Tanzania mmekubaliana kwamba mta-import mbaazi kutoka kwao, sasa wakulima wetu wamelima hawana soko, tunaomba muweke ban kwenye importation ya mbaazi kutoka nchi za Afrika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tuliaothirika sio Tanzania peke yake ni pamoja hata na jirani zetu Malawi ambao wanalima kuliko sisi. Kwa hiyo, sasa usiwe wimbo wa kuikosoa Serikali; mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na ndiyo maana naunga mkono jibu la Naibu Waziri alilosema kwamba hata na sisi tujifunze kula mbaazi, sisi ni Wabunge tumeaminiwa lazima tujiongeze kwenye kudadavua mambo, hajamaanisha ukapike nyumbani kwako, tu-cultivate tabia ya sisi wa kwanza kutumia bidhaa tunazozizalisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nikaenda mbali nikasema ili Serikali muwe mfano, basi kule magerezani na mashuleni tunapeleka vyakula tuwafundishe kule kula mbaazi instead of maharage ili ninyi muanze kama mfano. Sisi tunapoenda Mjimboni mwezi mtukufu wa Ramadhani watu mnaongelea mafuta, sukari tuseme na mbaazi, hata kiafya ni nzuri. Kwa hiyo, lazima sisi tuwe mfano, bidhaa zetu sisi tuwe watumiaji wa kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ndicho kinachotukuta, ufuta wote tunautoa nje kwa sababu hatujui umuhimu. Unaambiwa duniani hata hii alizeti tunaongea cholesterol free it’s not true, mafuta ambayo hayana rehemu kabisa ni mawili, mafuta ya ufuta na mafuta ya nguruwe (pig fat), that is the truth. Kwa hiyo, leo hii tunasafirisha ufuta wote kwenda nje kwa sababu hatupo aware kuhusu... (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi naunga mkono hoja nawashukuru sana.