Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuchangia Wizara hii ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, napenda nimpongeze Mheshimiwa Joseph Mbilinyi na nimpe hongera kwa kuongeza CV ya siasa katika Taifa hili. Tunamwambia karibu tuendelee na kulijenga Taifa hili, mapambano yanaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo mengi ya kuzungumza kutokana na kwamba mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira, yapo mengi nayofahamu na Waziri wa Viwanda anafahamu nini ambacho nimekuwa nikikidai katika Kamati hiyo. Kwa leo nataka nibebe angalau hoja moja au mbili kutokana na muda na naomba nizungumzie kuhusu uhaba wa sukari nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hitaji la sukari kwa mwaka ni tani 440,000, uwezo wa viwanda vyetu ni kuzalisha tani 3,000 pekee. Hivi navyozungumza bei ya sukari kwa mfuko wa kilo 50 ni Sh.110,000 lakini kila mwaka tunakuwa na upungufu wa sukari karibia tani 140,000 sawa na asilimia 32.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilitoa vibali kwa ajili ya kuagiza sukari kwa wafanyabiashara kwa lengo la kukidhi mahitaji ya Taifa letu au kwa maana nyingine kwa walaji. Nikizungumzia suala la bei ya Brazil, sukari kwa bei ya Brazil ni sawa na dola 3,090 sawa na Sh.860,000 na hiyo ni pamoja na kodi asilimia 25 na VAT asilimia 18. Kwa bei hii sukari ilipaswa kuuzwa Sh.65,000 na siyo Sh.110,000 au ingeweza kuuzwa Sh.80,000 maana wao kule wananunua kilo 50 Sh.65,000 maana yake wangeweza kuuza hapa Sh.80,000 na isiwe Sh.110,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumza haya kwa masikitiko kwa sababu kila kukicha tunaisikia Serikali inasema ni Serikali ya wanyonge. Kama Serikali ni ya wanyonge ni kwa nini Serikali inawauzia wananchi sukari kwa bei ya juu kiasi hiki? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ina maana ukigawanya hapa ni kama wanauza kwa kilo Sh.3,000. Kama Serikali ni ya wanyonge, kwa nini basi Watanzania wasipate sukari kwa Sh.1,500 kwa kilo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilitoa vibali watu waagize sukari kwa lengo la kuleta ushindani wa soko. Cha kushangaza ni kwamba sukari ile ile ya ndani na nje inauzwa bei moja. Sukari kwa bei ya ndani inauzwa Sh.110,000 na sukari ya nje inauzwa bei ileile. Sasa najiuliza, ni kwa nini Serikali ilitoa vibali kwa walewale wenye viwanda badala ya wafanyabiashara wengine ili kuleta ushindani wa soko na kuleta tija kwa walaji? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja anipe majibu, kwa nini Serikali haikutoa vibali kwa wafanyabiashara wengine na ni kwa nini imetoa kwa wafanyabiashara walewale ambao sisi tunasema sukari ambayo wanazalisha wao haikidhi na ndiyo maana Serikali iliamua kutoa vibali ili tukidhi hitaji la Watanzania? Kwa hiyo, naomba majibu atakapokuja Mheshimiwa Waziri wa Viwanda. (Makofi)