Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia Wizara hii kwa mara ya tatu sasa, toka mwaka 2016, ni Wizara ambayo sijaacha kuichangia.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2016 mchango wangu ulijikita kwenye kufungamanisha sekta ya kilimo na sekta ya viwanda. Moja ya jambo kubwa ambalo tulikuwa nalo wakati ule ilikuwa ni mgogoro wa sukari ambao sasa unazungumzwa na tulikuwa pia na mgogoro wa kuhusu mafuta ya kula ambao bado tunauzungumza.

Mheshimiwa Spika, Wabunge wa Mikoa ya Dodoma, Manyara na Kigoma ni Wabunge ambao tukipambana vilivyo tunaweza kabisa kuiondoa nchi yetu na aibu ya kuagiza mawese kutoa nje. Migogoro ambayo tunaizungumza kila siku hapa na mijadala ambayo tunayo na wewe mwenyewe juzi ulikuwa mkali sana ni kwa sababu ya mawese kutoka nje. Tuna uwezo wa kuzalisha mawese lakini Serikali haijaweka mkakati wowote ule wa kuhakikisha kwamba tunajitosheleza na tunaweza tukauza nje. Haijaweka mkakati wowote ule wa kuhakikisha kwamba tunaongeza uzalishaji wa alizeti, tuweze kuchakata hapa na tuondokane kabisa na hii aibu ya kuagiza mawese kutoka Malaysia, watu ambao walikuja kuchukua mbegu Kigoma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, huu ni mwaka wa tatu sijaona katika mpango wowote wa Serikali kuhusiana na jambo hili na bado tunabishana na kulumbana na kushutumiana kwa uagizaji wa mawese. Hili ni jambo ambalo linapaswa liwe ni aibu hata kulizungumza katika Bunge hili kwa sababu tuna alizeti, tuna mawese Kigoma na maeneo mengine kama Kyela yangeweza kabisa kumaliza matatizo kama haya.

Mheshimiwa Spika, mwaka jana nilizungumza fungamanisho kuhusu miradi mikubwa inayoendelea nchini na viwanda na hasa hasa niliangalia suala la ujenzi wa reli na jinsi ambavyo tunaagiza malighafi za ujenzi wa reli kutoka nje. Leo umemsikia Waziri hapa anazungumza, bado tunalipa fidia Mchuchuma na Liganga. Leo umemsikia Waziri anazungumza kwamba wamekwenda wamefungua kiwanda cha nondo wapi, kiwanda cha nondo sehemu nyingine, nondo zote hizi malighafi zake ni kutoka nje na sisi tuna chuma Mchuchuma na Liganga miaka yote tunazungumza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wewe ni Mbunge tangu mwaka 2000 unakumbuka, tangu mwaka 2000 tunazungumza Mchuchuma na Liganga, leo Waziri anazungumza kulipa fidia Mchuchuma na Liganga. Sisi ni watu wa namna gani? Kuna takwimu moja inaonesha kwamba 40 percent ya Watanzania ni stunted, inawezekana humu 40 percent of us ni stunted, kwa sababu tunaongea vitu vilevile, miaka yote tunakumbushana, nothing happens. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo hii kweli inaingia akilini, tuna chuma na makaa ya mawe yamejaa pale Ludewa tunampa mkandarasi kazi ya kujenga reli, vyuma vinatoka Uturuki, India, China, kweli? Wenzetu Kenya wanajenga reli na wenyewe wanaagiza hukohuko wakati tungeweza kuwauzia. Zambia wanajenga reli kuunganisha Angola na Zambia, tungeweza kuwauzia chuma, kwa kweli mimi sioni what we are doing. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwaka 2016 Serikali ilikuja hapa na mpango unaitwa C2C, Cotton-to-Clothing, nimeangalia hotuba ya Waziri hapa, hata kulizungumza neno hilo ameona aibu. Unaondoaje umaskini bila viwanda vya nguo? Niambie nchi gani? Uingereza ambayo ni moja ya nchi kubwa umasikini wake umeondolewa na viwanda vya nguo na hawakuwa na pamba walikuwa wanaagiza pamba kutoka kwenye makoloni yao. Hata kuzungumza Mheshimiwa Mwijage Cotton-to-Clothing, agenda yenu wenyewe na ulikuja hapa ukatamba na vitabu kama ulivyovileta leo, where is it? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, eneo kubwa ambalo napenda kuliongelea, nimalizie dakika zangu za mwisho ni biashara ya nje. Tunazungumza viwanda lakini kwa miezi 24 iliyopita Serikali hii ya Awamu ya Tano imesababisha hasara ya nchi yetu ya mauzo nje ya thamani ya dola bilioni moja na siyo takwimu zangu, ni takwimu zao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, angalia ukurasa unaozungumzia China, ukurasa wa 51, mauzo yetu nje China yameporomoka. Nasoma takwimu, China mauzo nje yameporomoka kutoka dola milioni 356 mwaka 2016 mpaka dola milioni 217 mwaka 2017, kutoka takwimu za Serikali. Japan, mauzo yetu nje yameporomoka toka dola milioni 140 mpaka dola milioni 75.

Mheshimiwa Spika, lakini zaidi tumeshindwa hata kuuza mbaazi India. Waziri alikwenda India amesema amezungumza, mimi sina hakika kama Waziri kweli alikwenda kuzungumza na Waziri mwenzake lakini biashara ni diplomasia. Mwigaje huwezi wewe unazunguka kuna viwanda, Naibu wako anazunguka na viwanda, international trade ni Foreign Affairs. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, juzi Vice President alikuwa London, Modi alikuwa London, mmeshindwa kuseti appointment ya Vice President na Modi wakazungumza tukatatua tatizo la mbaazi? Mbaazi bei imeporomoka kutoka Sh.3,000 mpaka Sh.150 kwa kilo. Mwezi Machi nimezunguka kwenye kata 16 nchi hii nimekuta watu wanalia mbaazi zimo ndani. Waziri Mstaafu Nape alizungumza hapa, alimuuliza Naibu Waziri, Naibu Waziri akasema kwamba tutakula, no it is foreign trade! It is about forex! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nchi hii tunaagiza nje vitu tunahitaji fedha za kigeni, mbaazi, choroko, giligilani, zilikuwa zinatupa dola milioni 224 kuuza India mwaka 2016, mwaka 2017 ikaporomoka dola milioni 131, mwaka 2018 sasa hivi dola milioni 75, what are you doing? Unapopoteza hizi forex utanunua mafuta na nini kwa sababu inabidi uagize. What will you buy mafuta with?

Mheshimiwa Spika, mimi nashindwa kuelewa what are we doing. Wizara ya Viwanda na Biashara that part ya biashara especially foreign trade hamna, tumepoteza one billion dollars in the span of 24 months, ni sawasawa na kupoteza kila siku shilingi za Kitanzania bilioni tatu in the last 24 months, you are still here Mwigaje, why don’t you just quit? Umeshindwa kazi. You can’t run Wizara ya Viwanda na Biashara as if you are running TAMISEMI, it is diplomacy, it is about going out getting markets. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo Malaysia kule a friend of Tanzania has been elected as a new Prime Minister, Mzee Mahathir, a very close friend of Mwalimu Nyerere, go there immediately, get the markets. Hamuwezi mkajidanganya na viwanda vya cherehani mkadhani kwamba you save this country! Foreign trade is power.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, haiwezekani sisi tukakosa soko India. The majority ya Wahindi ambao unawaona hapa Tanzania they are from Gujarat, Modi is from Gujarat, use that, talk to them! Hebu tuwaokoe hawa wakulima wa mbaazi, wakulima wa giligilani, giligilani imeshuka bei, mbaazi imeshuka bei, choroko imeshuka bei na dengu imeshuka bei, what are you doing?

Mheshimiwa Spika, ahsante.