Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kushukuru kwa kunipa nafasi, lakini pia nitumie nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu na watendaji wote wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa kazi nzuri wanaoendelea kufanya. Pamoja na pongezi hizo niliona na mimi nisimame nitoe mchango wangu kidogo kwenye Wizara hii hususani pale ambapo michango ya baadhi ya Wabunge wenzangu ilipojielekeza kwenye kujaribu kuangalia kipi ni kipaumbele muhimu zaidi kati ya kuwekeza kwenye kununua bombardier, ama kuwekeza kwenye kutoa huduma za maji kwa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia sana katika muktadha wa maendeleo, unaweza ukapata changamoto kwamba kipi kianze na unaweza ukaingia kwenye mtego wa hadithi ya kuku na yai kwamba kipi kinaanza? Kuku ama yai ama yai ama kuku na matokeo yako unaweza kujikuta unashindwa kufanya uamuzi. Lakini kwa wale tuliopata bahati ya kusoma masomo ya kuweka vipaumbele (priority setting) na masomo ya usawa tunakubaliana kwamba cha msingi zaidi ni namna tu ya kuweka utaratibu wa kuweza kufikia malengo unayoyakusudia, na wale usiingie kwenye mtego wa kuamua kipi kianze kuku ama yai na vitu kama hivyo. Kwa hivyo, kweli hili la kwamba tunanunua bombadier ama tunawekeza kwenye maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kwanza napenda nilihakikishie Bunge lako tukufu kwamba sekta ya maji ni katika sekta zinazopewa kipaumbele cha hali ya juu katika nchi yetu na kuna uwekezaji mkubwa unafanyika kwenye sekta hii na hata hili linadhibitika kwenye bajeti ya mwaka huu kuna zaidi ya bilioni mia sita tisini na saba zimetengwa kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maji hapa nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia ukisoma ukurasa wa saba wa kitabu cha Mheshimiwa Waziri utaona anaeleza kwamba malengo kwenye sera ni pamoja na kuwa asilimia 85 ya vijiji vya Tanzania vinapata maji safi na salama kufikia mwaka 2020; na kwamba mpaka leo hii utekelezaji umeshavuka lengo la asilimia 85 ambapo utekelezaji umefikia asilimia 85.2. Japokuwa kuna mapungufu madogo madogo kwenye hiyo miradi, na kwamba kati ya utekelezaji huu wa kiwango hiki cha asilimia 85 ni asilimia 58.7 tu ndio ambao wanaweza kupata maji kutokana na miradi mbalimbali iliyotekelezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninachokiona hapa ni kwamba, zifanyike jitihada za makusudi za kuongeza tija na ufanisi kwenye utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maji, lakini si kwamba hakuna uwekezaji unaofanywa kwenye sekta ya maji na hivyo hatuwezi kufananisha uwekezaji kwenye ununuzi wa bombardier against ule wa kuwekeza kwenye huduma za maji hapa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo napenda kusema kwamba hakuna makosa yaliyofanyika kwenye kuwekeza kununua ndege za bombardier na ninampongeza Mheshimiwa Rais, kwa uamuzi huu mahususi wa kuamua kuifufua sekta ya Utalii kwa kuwekeza kwenye ununuzi wa bombardier.

Ninachopenda kumalizia kwenye mchango wangu ni kwamba Mheshimiwa Rais anapaswa apongezwe.

KUHUSU UTARATIBU . . .

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ninachojaribu kusema ni kwamba napenda kutumia nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuamua kwa dhati kabisa na kwa pesa zetu wenyewe kulifufua Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kwa kuwekeza kwenye ununuzi wa ndege za bombardier na dreamliner na pengine na airbus ziko njiani zinakuja.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninavyozungumza hapa, wenzetu wa Ethiopia wamenunua ndege kumi, wameweka order za bombardier kumi kwa ajili ya kuendelea kujitanua na kuboresha sekta yao ya utalii na sisi hatuwezi kubaki nyuma. Tanzania inaongoza kwa kushika nafsi ya pili kwa vivutio vya maliasili duniani lakini bado hatujavitumia ipasavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, mapungufu tuliyo nayo ni pamoja na kuwa na miundombinu mibovu, ni pamoja na kukosa national career ambayo ingeweza kusafirisha watalii kutoka kwenye nchi zao kuja hapa ndani, lakini pia kuwatoa hapa ndani kutoka kwenye kituo kimoja kwenda kituo kingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo jitihada za kufufua Shirika la Ndege la Taifa zinapaswa kuungwa mkono na sisi Wabunge ambao ni wawakilishi wa wananchi. Hivyo nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa jitihada hizo, na sisi wa sekta ya utalii tunafurahia sana lakini tuna kereka sana watu wanavyoitupia mawe idea hii ya Mheshimiwa Rais ya kuwekeza kwenye manunuzi ya bombardier.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia tunafarijika sana na jitihada zinazofanywa na wenzetu kwenye sekta nyengine kama sekta ya ujenzi, kwa kufungua barabara shirika la reli pamoja na kujenga viwanja vya ndege. Zote hizi zinaenda kutia chachu ya kukua kwa sekta ya utalii ambapo katika nchi hii ipo katika sekta ya utalii.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana naunga mkono hoja.