Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. OMAR A. KIGODA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa napenda kumpongeza Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya pamoja na Serikali yake. Pili, nawapongeza sana Mheshimiwa Waziri wa Maji na Naibu wake kwa mapambano makubwa ya kuhakikisha ufumbuzi wa maji unapatikana. Vilevile nampongeza Katibu Mkuu na Naibu wake kwa kuongoza Wizara vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, nina ushauri kidogo kwa Wizara ya Maji na Umwagiliaji. Lazima sasa tubadilike na kuhakikisha watendaji wote wa Wizara na Idara za Maji hawafanyi kazi kwa mazoea. Mfano, kwenye Jimbo langu kuna watu wana zaidi ya miaka 30 wako eneo moja; kwa vyovyote mtu kama huyu hawezi kuwa na performance nzuri. Lazima sasa hivi watu wote walioajiriwa wapimwe utendaji wao (performance) ikiwezekana kwa kila mwaka kwamba wamefanya engineer katika Wilaya, unakaa miaka kumi hakuna chochote ulichofanya, lazima wapewe performance time.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaelewa kuna tatizo la upatikanaji wa fedha, ila hata hiyo hela ndogo inayopatikana kama tunapata watendaji wabunifu, inaweza kupunguza shida ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuwaambia Mheshimiwa Waziri na Naibu wake kwamba haya malalamiko wanayopata leo ni kwa sababu ya utendaji wa mazoea uliopita. Mfano, ni juzi Mheshimiwa Rais alivyompigia Katibu Mkuu wa Wizara mpaka leo tumeambiwa wataalam wameshakwenda na kazi imeanza. Hii inaonekana kabisa watendaji wa kwenye eneo husika hawakuwa makini (ufanyaji kazi kwa mazoea).

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho nawapongeza sana kwa kupata hela ya fidia. Hakika kuna miradi mingi itanyanyuka.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.