Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu kwa kazi nzuri wanayoifanya kwenye sekta ya maji. Nawapongeza kwa sababu upatikanaji wa maji umeongezeka pamoja na kuwa bado yapo maeneo ambayo hawajapata maji safi.

Mheshimiwa Naibu Spika, inasikitisha kuona kuwa Serikali inaweka mikakati mikubwa ya kuongeza upatikanaji wa maji nchini, lakini maji mengi sana yanapotea sababu ya uchakavu wa miundombinu. Hili ni tatizo kubwa, inafifisha kazi nzuri inayofanywa kwenye sekta ya maji. Je, katika bajeti hii zimetengwa fedha za kutosha kuboresha au kukarabati miundombinu ya maji iliyochakaa?

Mheshimiwa Naibu Spika, ziko Taasisi na Idara za Serikali ambazo wanatumia maji, lakini hawalipi ankara za maji, inabidi kila mtumiaji wa maji alipe maji kama Mheshimiwa Rais alivyoagiza. Kama hawalipi wakatiwe huduma. Na mimi naona wakatiwe ili walipe kusudi kuzipa nguvu Mamlaka za Maji ziweze kujitegemea.

Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali kwa mpango wao wa kuiweka Bukoba Mjini kwenye mpango wa kuandaa mfumo wa kuondoa maji taka. Tatizo hili limekuwa la muda mrefu. Taka hizi hutiririsha maji machafu kwenye mfereji hadi ziwani. Nawapongeza French Development Agency- AFD. Je, mradi huu utaanza lini?

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.