Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa taarifa za uchangiaji wa bajeti ya Maji kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Bwawa la Mindu nimeona katika kitabu cha Waziri anasema yupo kwenye majadiliano na Wafaransa ili kufanya ukarabati wa bwawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa population ya Morogoro sasa Bwawa la Mindu haliwezi kuwa ni suluhisho sahihi, lazima Serikali ifikirie kuwa na bwawa lingine ambalo litasaidiana na Bwawa la Mindu ili kutosheleza wananchi wa Manispaa ya Morogoro pamoja na viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Bwawa la Kidunda, fidia zilizotolewa na Serikali kwa wananchi ni ndogo, hazikidhi na bado yapo malalamiko ya wananchi wa ndani kupunjwa. Ni vyema Wizara ikajiridhisha na fidia hizo hata kama zimefanywa na evaluator wa Serikali lakini bado mradi huu ili ufanikiwa lazima Wizara ijenge mahusiano na wananchi ambao watakuwa ndio wanufaika na walinzi wa mradi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu gharama za ku-drill visima, suala la kupeleka maji kwa wananchi ni jukumu la Serikali, lakini cha kushangaza sana, mtu anakosa huduma ya maji anaamua kukusanya pesa ili kuchimba kisima; gharama za kufanya survey na kupata kibali cha kuchimba maji ni shilingi 250,000. Pia kila mwaka wananchi waliochimba kisima wanalazimika kulipa shilingi 250,000 kila mwaka, hiyo siyo sawa. Kama mwananchi amechimba kisima, analipia umeme kusukuma maji, automatically kwenye umeme analipa kodi, kwenye jenereta na analipa kodi ya dizeli kusukuma maji. Hivi kwa nini Serikali inalipisha kodi nyingine tena shilingi 250,000? Hii haikubaliki. Watu wa bonde wanapaswa kuangalia upya malalamiko hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kuendelea ku-harass vijana na akinamama ambao wanaweka pump za maji ili kumwagilia mboga mboga katika mashamba ambapo Morogoro akina mama na vijana walinyanganywa pump zao za umwagiliaji tu wanatakiwa kulipa kodi maji ambayo ni ya mto yanayoenda kupotea baharini.

Mheshimiwa Naibu Spika, watu wanaamua kuya- utilize maji hayo ambayo yangeweza kupotea badala yake wananyang’anywa pump za umwagiliaji, tena vikundi vya akina mama wenye mkopo benki. Hii siyo sawa. Pengine Serikali ingeweza kusubiri wavune mboga mboga na walipe ushuru sokoni badala ya kuvi-harass vikundi vya wanawake na vijana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kipaumbele cha Serikali bado siyo maji na ndiyo maana fedha zinazotengwa haziendi kwenye Wizara na hii imezua mashaka baada ya kubaini baadhi ya maeneo. Mfano, Mkoa wa Katavi umepelekewa miradi mingi kuliko mikoa mingine, hii haikubaliki. Lazima miradi hii ya visima igawanywe kwa usawa kwa kuwa tatizo la maji ni la nchi nzima.