Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ESTHER L. MUDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anazozifanya Mwenyezi Mungu ambariki sana. Pili, nampongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri kwa hotuba yao nzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, naishukuru sana Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi kwa kutenga fedha shilingi bilioni 15 kwa ajili ya kuvuta maji toka Ziwa Victoria kuleta Simiyu, pamoja na Wilaya zake za Busega, Bariadi, Itilima, Meatu na Maswa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa nianze kuchangia, kuna Mradi wa Chujio Wilaya ya Maswa ni wa muda mrefu sana umeshindwa kabisa kukamilika. Mkandarasi kila akiongezewa muda ameshindwa kabisa kukamilisha, wananchi wa Wilaya ya Maswa wakiendelea kunywa maji siyo safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inakigugumizi gani cha kuvunja mkataba na kumpa au kufunga mkataba na mkandarasi mwingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja.