Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Naibu Spika, kuna shida kubwa sana ya malisho ya mifugo yetu Jimbo la Ushetu kwenye Kata za Ulowa, Ubagwe, Ulewe, Nyankende na Idahina na Mheshimiwa Waziri atakumbuka tumepewa muda wa ukomo 15 Juni, 2016 tuwe na eneo mahsusi la malisho kutokana na kauli ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili ya tarehe 2 Aprili, 2016. Nimesoma hotuba na jedwali Na.12 sijaona kuwa tumetengewa maeneo ya malisho. Naomba ufafanuzi hali ni mbaya na tuna eneo la misitu ya Usumbwa na pori la Ushetu – Ubagwe ambalo linaweza kutuondolea adha na mgogoro wa wafugaji na wakulima wa Jimbo la Ushetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo haya yana ukubwa ufuatao, Usumbwa kilomita 360 na Ushetu – Ubagwe kilomita 310. Idadi ya ng‟ombe peke yake Jimbo la Ushetu inakadiriwa kuwa zaidi ya 300,000. Hivyo, naomba ulitolee commitment jambo hili na itapendeza pia ukitoa kauli juu ya maeneo yote yanayozunguka hifadhi ya Kigosi – Muyowosi. Ahsante.