Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Amina Nassoro Makilagi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. AMINA N. MAKILAGI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchukua nafasi hii kukushukuru wewe na nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kusimama na kutoa mchango katika hoja hii muhimu ya maji na uhai.

Mheshimiwa Naibu Spika, pongezi, nichukue nafasi hii kumpongeza Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote wa sekta hii ya maji na umwagiliaji kwa kazi nzuri waliyofanya kuandaa randama na hotuba hii na kuiwasilisha vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninawapongeza Waziri na timu yake kwa jinsi wanavyojituma kufuatilia kero za maji na kuzipatia ufumbuzi. Hakika ninaungana na nukuu ya usemi wa Mzee Makamba kwamba; “ujana siyo sifa na uzee siyo sifa, sifa ni hapa kuna kazi nani anaiweza.” Hongera sana Waziri pamoja na umri wako kazi ya sekta hii unaiweza na umefanya vizuri sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali kwa kujenga miundombinu ya maji mijini na vijijini kwa kiasi kupunguza tatizo la maji hasa mijini ukiwemo na mradi mkubwa wa kupeleka maji katika Jiji la Dar es Salaam na miji mingine hapa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na pongezi hizi, nashauri zitengwe fedha kwa ajili ya kujenga miundombinu ya maji katika Jiji la Dar es Salaam na katika miji mingine ili kuondoa tatizo la upotevu wa maji na mradi wa maji wa visima vya Mpera, Kimbiji na Ruvu ili uwanufaishe wananchi wa Mkoa wa Pwani.

Mheshimiwa Naibu Spika, Miradi ya Maji Vijijini iliyofadhiliwa na Benki ya Dunia pamoja na kuipongeza Serikali, Benki ya Dunia kwa kutafuta fedha na kujenga miundombinu ya miradi ya maji katika vijiji na katika kila Halmashauri za Wilaya na kuwezesha wananchi/wanawake kuondokana na kero ya maji. Pamoja na pongezi hizi, miradi ya maji ya vijiji kumi katika baadhi ya Halmashauri za Wilaya haikusimamiwa vizuri na baadhi ya miradi haikukamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali, ningependa kujua:-

(i) Ni vijiji vingapi miradi imekamilika na wananchi wanapata maji na katika Halmashauri zipi?

(ii) Ni miradi mingapi imekamilika lakini maji hayatoki na nijue tatizo ni nini na ufumbuzi wake ni nini?

(iii) Miradi mingapi iko katika hatua za ujenzi na itakamilika lini na iko katika Halmashauri ya Wilaya gani na itakamilika lini?

(iv) Je, Serikali imejipangaje katika kuhakikisha miradi ambayo ilikamilika na haitoi maji inatoa maji na miundombinu ya miradi ambayo haijakamilika. Nini mipango ya kukamilisha miradi hii?

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji Mugango wa Kiabakari Butiama, mradi wa kujenga miundombinu Mugango - Kiabakari - Butiama ni mradi ambao ulipangwa kutekelezwa miaka mingi zaidi wakati wa Waziri wa Maji Ndugu Mwandosya, tangu wakati huo hadi sasa maelezo ni kwamba mradi huo utajengwa kwa fedha za wadau BADEA na kwamba zimekwishapatikana USD 32.

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa miundombinu ya kupeleka maji mpaka Butiama kwenye kaburi la Baba wa Taifa kwa kweli limekuwa ni jambo linalotia simanzi kubwa sana kwa wananchi wa Wilaya ya Butiama kwa sababu mradi huu hautekelezwi kama ulivyopangwa. Swali:-

(a) Ningependa kujua hivi tatizo hasa ni nini mbona ujenzi wa mradi huo hauanzi?

(b) Je, fedha hizo kutoka BADEA USD 32 zipo na ziko katika akaunti gani na zimeingia lini?

(c) Mkandarasi aliyeteuliwa kujenga miundombinu ya maji ya mradi huu wa Mgango - Kiabakari - Butiana ni nani na anaanza kazi lini?

(d) Ningependa kujua pia kama mradi huu utakamilika utawahudumia pia wananchi Kata ya Buruma, Butuguli na Muliyaza kwa sababu mradi huu miundombinu yake itapita katika baadhi ya vijiji vya kata hizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri, ningependa kujua kama mradi huu utawahudumia wananchi wa Kata ya Mgango, Kiriba na Tegeruka maeneo ambayo yako karibu sana na chanzo cha Mradi wa Maji cha Mgango.

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa miundombinu ya maji katika maeneo yanayozungukwa na maziwa na mito; pamoja na kuipongeza Serikali kwa kujenga miundombinu ya maji katika vyanzo vya maji ya maziwa na mito mfano, Ziwa Victoria linatoa maji mpaka Tabora na Wilaya zake. Ningependa tutumie fursa ya mito na maziwa kujenga miundombinu ya maji katika:-

(a) Mkoa wa Mara unazungukwa na Ziwa Victoria, Mto Mara na Mto Sisiti.

(b) Mkoa wa Mwanza tupeleke maji katika Wilaya zote kwa kutumia maji ya Ziwa Victoria na Mto Sibiti.
(c) Mkoa wa Geita - Ziwa Victoria.

(d) Mkoa wa Simiyu – Ziwa Victoria na Mto Simiyu.

(e) Mkoa wa Kagera – Ziwa Victoria, Mto Kagera na mito mingine.

(f) Mkoa wa Ruvuma – Ziwa Nyasa Mkoa wa Ruvuma, Mbeya, Songwe na Ruvuma na Mkoa wa Katavi na Kigoma tutumie Ziwa Tanganyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, ijengwe miundombinu ya maji katika mikoa ya Pwani, Dar es Salaam, Lindi, Tanga, Mto Rufiji utosheleze maji katika Mkoa wa Pwani, Dar es Salaam na Lindi. Mikoa ya Morogoro na Mto Kilombero, Mkoa wa Dodoma Mto wa Mtera na Mto Zigi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo cha umwagiliaji, pamoja na kuipongeza Serikali kwa kazi nzuri ya kujenga miundombinu ya umwagiliaji, naishauri Serikali yafuatayo:-

(a) Kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji ili kuongeza kiwango cha uzalishaji wa chakula na biashara hasa katika maeneo ambayo hayapati mvua za kutosha. Pia tuwe na uhakika wa chakula bila kutegemea mvua.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa kilimo Bugwema Irrigation ningependa kujua:-

(a) Bugwema Irrigation inamilikiwa na nani?

(b) Je, kuna mkakati gani kuhakikisha mradi huu unafufuliwa na unaleta tija kwa wananchi wa Musoma Vijijini na Mkoa wa Mara na Taifa kwa ujumla na hasa Wilaya ya Musoma Vijijini, Butiama, Bunda na Wilaya ambazo zimekuwa zikikumbwa na ukame. Vilevile ardhi kuchoka na pia kuna ugonjwa wa mihogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji Manispaa ya Musoma pamoja na kuipongeza Serikali kwa kujenga miundombinu ya maji na kuwawezesha wananchi kuweza kupata maji kwa kiwango kikubwa ijengwe miundombinu kwa ajili ya kufikisha maji katika vijiji vya Kata ya Nyakanga, Bukabwa Wilaya ya Butiama na Kata ambazo ziko karibu sana na chanzo cha maji Musoma Mjini na miundombinu iliyojengwa ikiboreshwa kidogo inaweza kufika huko. Pia nashauri mradi huu ufikishe maji katika vijiji vya Bukanga Kata ya Etalo, Kata ya Rifulifu, Nyegina na Nyakatende Wilaya ya Musoma Vijijini kwa sababu wako karibu na chanzo cha maji yanayokwenda Musoma Mjini. Naunga mkono hoja.