Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali kwa jitihada zake za makusudi inazochukua katika kuhakikisha wananchi wa Tanzania wanapata maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Waziri, Naibu Waziri na watendaji wote wa Wizara kwa kuhangaika kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama na kushughulikia miradi ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kuunganisha DAWASCO na DAWASA, ni jambo jema kwa watumiaji wa maji, ufanyike uchunguzi kwa DAWASCO na DAWASA kuhusiana na madeni, hasara na changamoto zote zilizopo katika taasisi hizo. Katika chombo hicho kipya kitakachoundwa watendaji watakaopewa kukiendesha wateuliwe wale ambao wana maadili na waaminifu ili kuepusha matatizo hasara na madeni ya lazima.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali na Wizara iendelee na juhudi zake za kutafuta fedha kwa madhumuni ya kuongeza miradi ya maji nchini ili Watanzania wapate huduma hiyo muhimu ya majisafi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja, ahsante sana.